Tuesday, January 27, 2015

USIKOSE HII KUTOKA DAR ES SALAAM LEO

Aliyekuwa waziri wa uchukuzi ambaye sasa ni aziri wa ushirikiano wa africa mashariki mh HARSON MWAKYEMBE akizungumza na wadau mbalimbali walojitikeza katika afla hiyo ya kutafuta fedha za kuendesha mkutano huo utakao fanyika mapema mwezi wa tatu
 Taasisi ya kimataifa ya uhudumiaji wa bidhaa na uchukuzi wa bidhaa CILT yani THE CHARTERD INSTITUTE OF LOGISTIC AND TRANSPORT Tawi la Tanzania imeandaa mkutano mkubwa nchini ambao utafanyika katika mkoa wa arusha tarehe 3 na 4 mwezi wa tatu mkutano wenye lengo la kuwakutanisha wadau mbalimbali wa maswala ya usafirishaji na uchukuzi kujadili changamoto mbalimbli katika secta hiyo.
Mwenyekiti wa CILT nchini Tanzania GEORGE MAKUKE akizungumza kuhusu mkutano huo na taasisi hiyo inavyofanya kazi. 
 Mkutano huo ambao utafanyika katika hoteli ya mount meru jijini arusha una mipango pia ya kuwakutanisha wanataaluma wa maswala ya uchukuzi na usafirishaji wa bidhaa ili kubadilishana uzoefu katika taluma hiyo.
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupata chai yenye lengo la kuchangisha fedha ambazo zitasaidia katika kuendesha mutano huo aliyekuwa waziri wa uchukuzi ambaye sasa ni waziri wa ushirikian wa Africa mashariki MH HARSON MWAKYEMBE amesema kuwa Tanzania kupata nafasi ya kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa kama huu ni fursa ya kipekee ambayo nchi inatakiwa kujivunia na kuitumia kujitangaza kimataifa.
 Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano huo ndugu ZAKARIA HANSPOP akizngumza.
 Amesema kuwa mkutano huo utawasaidia hasa vijana ambao wanasoma maswala haya kukutana na wazoefu katika fani hiyo na kubadilishana uzoefu jambo ambalo litawajengea uzoefu katika kazi zao pindi watakapoingia katika fani.
Aidha mwenyekiti wa CILT nchini Tanzania GEORGE MAKUKE anesema kuwa kwa sasa katika secta ya usafirishaj wa bidha nchini kumekuwa na watu ambao amewaita makanjanja ambao wamekuwa hawana weledi katika kazi na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi jambo ambalo amesema kuwa linafaa kupigwa vita mara moja.

Katika hatua nyingine mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mkutano huo ndugu ZAKARIA HANSPOP akizngumza katika hafla hiyo amewataka watanzania hususani wadau wa secta hiyo kujitoa katika kuufadhili mkutano huo kwani una manufaa makubwa katika ukuaji wa secta ya usafirishaji na uchukuzi nchini Tanzania

Picha tatu za juu zikionyesha washiriki mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo

No comments: