Tuesday, February 24, 2015

BALOZI WA CANADA ATAMBUA MCHANGO WA MKURUGENZI WA TAMWA,AMKABIDHI TUZO YA KUKOMESHA NDOA ZA UTOTONI

Balozi wa Canada Nchini Tanzania akimkabidhi tunzo Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania-TAMWA.
 Katika hali ya kutambua mchango mkubwa wa mkurugenzi mkuu wa chama cha wanahabari wanawake Tanzania TAMWA bi VALERIE MSOKA,balozi wa Canada nchini Tanzania ALEXANDER LEVEGUE leo amemkabidhi mkurugenzi huyo tuzo ya umahiri na utambuzi wa jitihada zake katika kukomesha ndoa za utotoni na vitendo vya ukeketaji nchini Tanzania.

Wapili kutoka kushoto ni Balozi wa Canada Nchini Tanzania Alexandre Levegue , Mkurugenzi mtendaji wa TAMWA Valerie Msoka, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Anna Maembe na wawakilishi mbambali kutoka mashitika ya umoja wa mataifa wa masuala ya wanawake.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo mkurugenzi huyo VALERIE MSOKA pamoja na kumshukuru balozi wa CANADA kwa kutambua mchango wake  amesema kuwa bado Tanzania inapita katika changamoto kubwa ya mwaswala ya ndoa za utotoni katika mikoa mingi kama shinyanga,Dodoma,mara na mikoa mingine ambapo amesema kuwa nguvu kubwa sana hasa kutoka serikalimi imahitajika katika kupigana kuokoa watoto wa kike ambao wanakumbwa na kadhia hiyo ikiwa ni pamoja na kutekeleza sheria ambazo zinawalinda watoto wa kike nchini.

Mkurugenzi wa TAMWA VALERIE MSOKA akizungumza na wanahabari kuhusu tukio hilo
Awali wakati akikabidhi tuzo hiyo balozi wa Canada nchini ALEXANDER LEVEGUE amesema kuwa licha ya Tanzania kupiga hatua katika kukabiliana na ndoa za utotoni na maswala ya ukeketaji amesema bado maeneo mengi jitihada kubwa zinahitajika ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya mila hizo ambazo zimekuwa zikiwatesha hasa watoto wa kike katika maeneo mengi nchini.

Wanahabari na wadau mbalimbali waliohudhuria katika shughulli hiyo
Katika hafla hiyo fupi pia ilihudhuriwa na katibu mkuu wa wizara ya maendeleo jinsia na watoto ANNA MAEMBE  ambapo pamoja na kumpongeza mkurugenzi wa TAMWA kwa tuzo aliyopata amesema kuwa jumla ya watoto 2 kati ya 5 nchini Tanzania wameolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18 huku hatari ya vifo na kuongezeka ugonjwa waq fistula na magonjwa ya kuambukiza yakiongezeka kwa kasi.

No comments: