Friday, April 10, 2015

CHUO KIKUU HURIA TANZANIA WAMUAGA RASMI PROFESA TOLLY MBWETE,ALIYEKUWA MAKAMU MKUU WA CHUO HICHO

Profesa TOLLY MBWETE makamu mkuu wa chuo kikuu huria Tanzania akipokea baadhi ya zawadi alizokuwa anapewa na wanafunzi pamoja na wanajumuiya wa chuo hicho tawi la temeke jioni bya leo wakati wa hafla ya kumuaga baada ya kiumaliza kipindi chake cha miaka kumi ya utumishi katika chuo hicho
 Wanafunzi pamoja na wanajumuiya wa chuo kikuu huria nchini Tanzania tawi la mkoa wa Temeke wamemuaga rasmi aliyekua makamu mkuu wa chuo hicho profesa TOLLY MBWETE ambaye amemaliza kipindi chake cha kuwa katika nafasi hiyo kisheria ambapo ni miaka kumi ya utumishi wa umma.

Profesa TOLLY MBWETE amewaaga rasmi leo wanajumuiya wa chuo hicho kikuu huria cha Tanzania tawi  la Temeke kufuatia kuteuliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vyuo vikuu barani Afrika. ambapo pamoja na mambo mengine ameonyesha kuwashuku wanafunzi pamoja na wafanya kazi wote wa chuo hicho waliokuwa naye pamoja katika kipindi chote cha utumishi wake.
Biongozi wa watu wenye ulemavu tanzania akimshiukuru profesa MBWETE kwa msaada ambao chuo chake kimekuwa kikiutoa kwa watu wenye ulemavu tanzania
Akizngumza na wanajumuiya hayo profesa MBWETE amesema kuwa
CHUO Kikuu Huria nchini (OUT) kipo katika mchakato wa kufanya maboresho ya mfumo wa utoaji wa elimu ambapo sasa kitaanzisha vyuo katika ngazi ya mkoa (College).
        
 Katika mabadiliko hayo chuo hicho pia kitafungua matawi katika ngazi ya wilaya kwa kushirikiana na   Halmashauri za wilaya.
                           
  Amesema mchakato wa mabadiliko hayo tayari umepata Baraka za Tume ya Vyuo Vikuu nchini na kwamba muda si mrefu OUT itaanzisha college katika ngazi ya mikoa.

         
 Kwa upande wake Mkurugenzi wa OUT mkoa wa Temeke Dk. Jacquiline Bundala amesema tangu kuanzishwa kwa kituo hicho mwaka 2007 chuo hicho kimepata mafanikio makubwa.
          
 Ameyataja baadhi ya mafanikio hayo ni pamoja na kuongeza idadi ya wanafunzi kutoka wanafunzi 258 waliokuwepo wakati huo hadi zaidi ya 600 waliopo sasa.


      Pamoja na mafanikio hayo Dk. Bundala pia amesema chuo hicho mkoa wa Temeke kinakabiliwa na tatizo la mtandao ambao ni nyenzo muhimu kwa ajili ya kujifunza.
       
Kata keki tule
    Kwa upande wake Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Huria mkoa wa Temeke Malimi Ntegwa ameutaka uongozi wa chuo hicho kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi ikiwemo tatizo la upatikanaji wa vitambulisho, sehemu za kujifunzia hasa wakati wa vipindi vya ana kwa ana.

PICHA NYINGINE ZA HAFLA HIYO ZIPO CHINI





No comments: