Thursday, April 16, 2015

LIVE COVERAGE--TIZAMA MBOWE ANACHOKIFANYA DAR ES SALAAM MUDA HUU

Mwenyekiti wa chama cha democrasia na maendeleo CHADEMA mh FREMAN MBOWE akiwasili katika viwanja vya PTA sabasaba jijini Dar es salaam kwa ajili ya ufunguzi wa mafunzo hayo maalum
 Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania CHADEMA Mh FREMAN MBOWE leo amezindua rasmi program maalum ndani ya chama hicho ya mafunzio kwa viongozi mbalimbali wa kanda ya Dar es salaam mafunzo ambayo yamelenga katika kuwajengea uwezo zaidi viongozi wa chama hicho na wale wanaotarajia kuwa viongozi baada ya uchaguzi ujao mwishoni mwa mwaka huu.
Akizindua mafunzo hayo jijini Dar es salaam leo mh FREMAN MBOWE ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa umoja wa katiba  UKAWA amesema kuwa lengo kuwa mafunzo hayo yameanzia katika mkoa wa Dar es salaam kwa kuwa ni ukweli usiopingika kuwa Mkoa huo ndio unaongoza kwa idadi kubwa ya wapiga kura nchini kwa takwimu za serikali ambapo wameona ni vizuri kuanzia katika mkoa huo na baadae kueneoa katika maeneo mengine.
Amesema kuwa malengo makuu ya mafunzo hayo ni kuwajenga viongozi bora, wenye weledi, wanaojua kuwatumikia wananchi waliowachagua,ambapo amesema mafunzo hayo yatatumika kama dira kuu ya chama hicho katika kuelekea kile alichokiita ushindi wa kishindo wa upinzani nchini katika uchaguzi ujao mwaka huu.

Amesema moja kati ya maazimio makubwa ya mafunzo hayo ni kuwajenga viongozi ambao watakwenda kushinda nafasi zote za uongozi katika majimbo manane ya mkoa wa dare s salaam na kufanyika hivyo kwa mikoa mingine nchinio Tanzania.
Umati mkubwa wa viongozi wa CHADEMA kutoka maeneo yote ya Dae es salaam waliohudhuria hapa
Akizngumza na mamia ya viongozi mbalimbali na watangaza nia waliojitokeza katika uzinduzi huo amesema kuwa lengo kuu la  UKAWA sio kugawana nafasi za uongozi kama inavyoendezwa bali ni kuwakomboa watanzania kutoka katika mikono ya wanyonyaji hivyo akawataka viongozi hao kuacha kufikiri sana kuhusu nafasi za uongozi bali wafikiri sana katika kuwakomboa wananchi
Mh MBOWE akizungumza
Aidha amesema kuwa baada ya kukamilika kwa mafunzo ndani ya mkoa wa dare s salaam viongozi na wakufunzi wa chama hicho watasambaa nchi nzima katika kueneza mafunzo hayo ambayo amesema kuwa kila kanda na kila sehemu magfunzo hayo yatafika lengo likiwa ni kujiandaa kuwa na sertikali bora ifikapo mwezi wa kumi.
Mwenyekiti MBOWE akizindua vitabu ambavyo vitatumika katika mafunzo hayo 
Katika hatua nyingine akizngumzia umoja wa katiba ya wananchi UKAWA amesema kuwa ni muda wa wanachama wa vyama hivyo kuwa na matumaini mapya na kuwa na moyo wa subira kwani viongozi wakuu wa vyama hivyo wanaendelea vizuri na vikao vya kukamilisha makubaliano yao kabla ya kuja na maazimio na majina ya wagombea wao ambapo amesema kuwa wale ambao wamekuwa wakisubiri wagombane waendelee kusubiri kwani umoja huo upo imara kulikp watu wanavyodhani.
TUNAOMBA RADHI KWA UONEKANI HAFIFU WA PICHA ZETU

No comments: