Friday, April 24, 2015

UMESKIA TIGO ILICHOKIZINDUA LEO DAR ES SALAAM--HII NI KUBWA KULIKO ZOTE TANZANIA,SOMA HAPA

Waziri wa mawasiliano,sayansi na Technologia Mh MAKAME MBARAWA akizngumza katika hafla hiyo iliyoandaliwa kampuni TIGO TANZANIA kwa ajili ya uzinduzi wa huduma hiyo mpya ya mtandao ya 4G katika ukumbi wa mlimani city Dar es salaam leo
 Kampuni ya simu za mkononi ya TIGO TANZANIA leo imezindua technologia mpya ijulikanayo kama 4G LTE ambao utaifanya kuwa mtandao wa internent mkubwa na wenye kasi zaidi nchini.
Akizungumza katika uzinduzi huo kaimu meneja mkuu  wa TIGO CECILE TIANO amesema kuwa kwa mara ya kwanza tena inaonyesha dhamira ya TIGO katika kuleta mabadiliko ya maisha ya kidigitali na kama vinara katika matumizi ya  tecnologia ya kisasa na ubunifu.
Kaimu meneja mkuu  wa TIGO CECILE TIANO akizngumza katika nhafla hiyo
Mtandao wa 4G LTE una kasi ya haraka katika kupiga simu yani SKYPE kuperuzi na kupakua vitu mbalimbali kutoka kwenye internent.Pia mtandao huo unaleta kitu kipya chenye huduma iliyo bora zaidi kwa urushwaji wa video au kufanya mikutano kwa njia ya mtandao.technologia hii mpya ina kasi ambayo ni mara tano zaidi ya technologia iliyopo sasa kwenye soko ijulikanayo kama 3G.
Mkurugenzi mkuu wa TCRA Profesa JOHN NKOMA akizungumza kwa niaba ya malaka hiyo ambapo ameipongeza kampuni ya TIGO kwa huduma bora hususani hiyo waliyoizindua leo
Kufwatia ongezeko kubwa la matumizi ya simu za kisasa nchini zijulikanayo kama smartphones technologia ya 4G itawezesha wateja wa TIGO kufurahia uzoefu huu wa kimataifa wa ongezeko la kasi na ubora wa upatikanaji wa internent kwa njia ya mtandao
Waziri akiwasili katika ukumbi huo leo
Amesema kuwa uzindiuzi wa leo umejumuisha maeneo ya mliman city na masaki lakini lakini mpango wa tigo ni kufikia maeneo yote ya Jiji la Dar es salaam ifikapo mwezi June kuhakikisha kuwa upatikanaji wa huduma hiyo  katika wilaya za kinondoni,ilala na temeke hususani maeneo ya Upanga,Tegeta,Mbagala,Tabata,Kimara,Mbezi,Ukonga,Salasala,Mikocheni,Msasani,Sinza,na kadhalika.
Wasanii wa maigizo tanzania KITALE na STANBAKORA walikuwepo kufwatilia shughuli hiyo maalum
Aidha ameongeza kuwa watazindua huduma hiyo katika Miji ya Arusha,Moshi,Dodoma,Morogoro,Mwanza,na Tanga ifikapo mwishoni mwa mwezi wa agosti.ambapo amesema hii itaifanya kampuni ya tigo kuwa mtandao mkubwa wa 4G nchini Tanzania.
Akizindua huduma hiyo ambayo ni mpya nchini waziri wa mawasiliano sayansi na technologia mh MAKAME MBARAWA amesema kuwa ni hatua kubwa sana imefanywa na kampuni ya TIGO kwa kuzindua huduma hiyo na inafaa kuigwa na makampuni mengine ili kuhakikisha kuwa Tanzania nzima inakuwa na huduma hiyo ambayo itawasaidia watanzania kwa namna moja ama nyingine.
VANESA MDEE msanii wa bongo flaver alikuwepo
Amesema kuwa nchi kama Tanzania kuwa na mtandao wenye uhakika na wa kasi ni fursa nzuri kwa vijana wake kujiajiri katika shughuli mbalimbali zinazohusiana na mitandao kwani inakuwa wamerahisishiwa kazi na kwa kuwa wana mtandao wenye kasi kama waliozindua kampuni ya TIGO ni raisi zaidi kufanya hivyo
RICH MAVOKO msanii maarufu wa bongo fleva alikuwepo na akapata nafasi ya kutoa burudani kidogo
Ameongeza kuwa serikali ipo pamoja na kampuni ya TIGO kwa kuhakikisha kuwa huduma hiyo inaena katika maeneo mengi ya nchi hadi vijijini ili lengo la kuifanya Tanzania iwe kama kijiji liweze kutimizwa kikamilifu ambapo litasaidia katika shighuli mbalimbali za kimaendeleo.
VABBESA MDEE akifwatilia muonekano wa video yake mpya unavyoonekana iwapo utaitizama katika mtandao wa 4G .
PICHA NYINGINE NYINGI KUTOKA KWENYE HAFLA HIYO ZIKO HAPA
























No comments: