Thursday, April 23, 2015

UMESKIA WALICHOKIFANYA MADIWANI WA HAI KWA MBOWE LEO--HIKI HAPA


Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Hai limewataka wataalamu wa ardhi kutoka nje ya kikao cha baraza hilo na kuleta taarifa sahihi zinazohusiana na ni hekari ngapi ambazo zinamilikiwa na halmashauri katika eneo la mashine Tools na ni majina ya wamiliki yafahamike.

Katika kumbukumbu amabazo zilizowasilishwa katika kikao cha baraza hilo zinaonyesha kuwa halmashauri hiyo inamiliki hekari 17 jambo ambalo lilitolewa maelekezo katika baraza lililopita na kusemekana ni hekari 27 ikiwa na maana kwamba taarifa ilikosewa kuandikwa.

Kati kikao cha leo kwenye kumbukumbu imeonyesha tena ni hekari 17 badala ya 22 ambapo Mh. Rajabu Nkya diwani wa kata ya Machame Mashari amehoji kuwa`` kuna aina fulani ya udanganyifu unaoendelea katika mashamba ya Mashine Tools tunamwomba afisa ardhi atuletee taarisa sahihi kabla ya kumalizika kwa kikao hichi na ikiwa inaonyesha majina ya wamiliki” ``kamati iundwe ili kubaini ukweli na uhalali wa mashamba hayo kwa wamiliki”

Baada ya mvutana wa muda mrefu iliundwa kamati ya watu sita watatu wakiwa ni waheshimiwa madiwani na watatu kutoka katika upande wa wataalam na kupewa wiki mbili katika kushughulikia jambo hilo.
katikati ya watatu waliovaa miwani ni Mbunge Viti maalum Jimbo la Hai Mh. Grace Kiwelu akisoma kabrasha la kikao cha Madiwani.
Mbunge wa Viti maalumu jimbo la Hai Mh. Lucy Owenya akichangia mjadala kuhusiana na hoja ya mapato ya halmashauri 60% kutengwa kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo ambapo awali madiwani walitaka kujua ni sababu gani zinakwamisha miradi mingine ya maendeleo katika wilaya kutoendelea hadi sasa
katikati ya picha ni mwenyekiti wa baraza la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Hai ndg. Clement   Kwayu, kulia ni makamu mwenyekiti Ally Mwanga na kushoto kwake ni mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Melkizedeck Humbe
Kushoto katika meza kuu ni Mkuu wa wilaya ya Hai Ndg. Antony Mtaka akizungumza katika kikao cha  baraza la madiwani  ikiwa ni mara yake ya kwanza mara baada ya kupata uhamisho toka Mvomero Morogoro kuja Wilaya ya Hai
 Picha zote na Davis Minja wa Pamojahabari.blogspot.com

No comments: