Wednesday, April 1, 2015

WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA TIGO WATEMBELEA WATOTO WA KITUO CHA SINZA MAALUM NA KUTOA ZAWADI YA PASAKA

Meneja mkuu wa Kampuni Tigo Tanzania Cecile Tiano, akimuangalia mtoto Godfrey Alistides wa kituo cha watoto wenye ulemavu cha Sinza Maalum akichora mfano wa basi,wakati wa hafla ya wafanyakazi wa kampuni ya Tigo walipotembelea kituoni hapo kutoa zawadi ya vitu mbalimbali kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka
 Tigo Tanzania jana imetoa vitu vya aina mbalimbali katika shule maalumu ijulikanayo kama Sinza maalumu iliyopo jijini Dar es salaam katika kusherehekea mapumziko ya sikukuu ya pasaka. Kampuni ya Tigo pia imelipia gharama ya matumizi ya umeme ya hapo shuleni kwa mwaka mmoja.
Meneja wa Uwajibikaji kwa Jamii kutoka Tigo Woinde Shisael, akiongea na waandishi wa habari, wafanyakazi wa Tigo na watoto wa Kituo cha Sinza Maalum wakati wa hafla ya kutoa vitu mbalimbali kwa kituo hicho chenye watoto wenye ulemavu. Wafanyakazi wa Tigo walijitolea vitu hivyo ikiwa sehemu ya kusheherekea sikukuu ya Pasaka pamoja na watoto.
 Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika shuleni hapo, Meneja mkuu wa Tigo Cecile Tiano alisema, vitu vilivyotolewa ambavyo ni pamoja na nguo, viatu, kinga na pedi ni ishara ya upendo na hali ya kujali kwa kampuni na wafanyakazi wa Tigo kutoa msaada kwa jamii ya watu wasiojiweza katika kipindi hiki cha sikukuu ya Pasaka.

Meneja mkuu wa Kampuni Tigo Tanzania Cecile Tiano, akiongea na waandishi wa habari, wafanyakazi wa Tigo na watoto wa Kituo cha Sinza Maalum wakati wa hafla ya kutoa vitu mbalimbali kwa kituo hicho chenye watoto wenye ulemavu. Wafanyakazi wa Tigo walijitolea vitu hivyo ikiwa sehemu ya kusheherekea sikukuu ya Pasaka pamoja na watoto. 
 "Pia tumetambua umeme wa kudumu ni moja ya hitaji muhimu sana hapa shuleni ndiyo maana Tigo imeahidi kulipa gharama zote za matumizi ya umeme ya hapa shuleni kwa mwaka mmoja kupitia Tigo Pesa," alisema Bibi Tiano. Shule maalum ya Sinza maalum inahudumia watoto 88 na vijana wenye umri wa miaka kati ya 9 na 25 ambao wanatoka katika familia zenye mazingira magumu au wanaoishi na mzazi moja au wanaishi na wazee.
Mwalimu Mkuu wa shule ya Watoto wenye ulemavu ya Sinza Maalum iliyopo Sinza Jijini Dar es Salaam akiongea na waandishi wa habari, wafanyakazi wa Tigo na watoto wa Kituo cha Sinza Maalum wakati wa hafla ya kutoa vitu mbalimbali kwa kituo hicho chenye watoto wenye ulemavu iliyofanywa na Wafanyakazi wa Tigo. Pembeni kushoto ni Meneja Rasilimali watu wa Tigo Catherine Olaka. 

Wasanii Christian Belle na Barnaba wakiwa pamoja na watoto wa Kituo cha Watoto wenye Ulemavu cha Sinza Maalum, wakati wa hafla ya kukukabidhi vitu toka kwa Wafanyakazi wa Tigo kwa kituo hicho kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka
 Meneja mkuu alifuatana na wafanyakazi wa Tigo na wasanii watano wa Bongo flava akiwemo msanii Fid Q,Menina, Christian Bella na Barnaba katika tukio ambalo lilikuwa la kusisimua na kupendeza kutokana na burudani ya moja kwa moja iliyotolewa na wanamuziki.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bw.Simon Milobo alitoa shukrani zake za dhati kwa kampuni ya Tigo,” hii sio mara ya kwanza kwa kampuni ya Tigo kutusaidia uwa wanakuja mara kwa mara kutusaidia tunawashukuru sana, naomba na makampuni mengine yaweze kujitokeza na kuiga mfano wa Tigo” alisema. 
Msanii Menina akiangalia vitu mbalimbali vinavyotengenezwa na watoto wa kituo cha Sinza Maalum, wakati wa hafla ya kukukabidhi vitu mbalimbali toka kwa Wafanyakazi wa Tigo kwa kituo hicho kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka. 

Mtaalam wa Mitandao ya Kijamii toka Tigo Samira Baamar akiwaonyesha jinsi ya kutumia iPad watoto wa Kituo cha Watoto wa Sinza Maalum, wakati wa hafla ya kukukabidhi vitu toka kwa Wafanyakazi wa Tigo kwa kituo hicho kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka. 

Msanii Fid Q akicheza nyimbo maalum ya kituo cha watoto wenye ulemavu cha Sinza Maalum na Mwalimu wa kituo hicho, wakati wa hafla ya kukukabidhi vitu toka kwa Wafanyakazi wa Tigo kwa kituo hicho kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka. 

Vifaa mbalimbali vilivyotolewa kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka kwa Kituo cha Sinza Maalum toka kwa wanyakazi wa Tigo. 

Msanii Christian Belle akionyesha watoto jinsi ya kutumia upawa wa kuchotea chakula






No comments: