Wednesday, April 29, 2015

WAISLAM WACHARUKA TENA,SOMA WALICHOKISEMA LEO JUU YA KAMATA KAMATA YA WAISLAM INAYOENDELEA NCHINI

Mwenyekiti wa jumuiya hiyo SHEKH MUSSA KUNDECHA akizngumza wakati wa akitoa tamko hilo leo jijini Dar es salaam 
 Wakati matukio mbalimbali ya kukamatwa kwa viongozi na waislam nchini kwa sababu za kujihusisha na ugaidi yakizidi kutokea Jumuiya ya taasisi za kiislam nchini Tanzania wameibuka na kulaani vitendo hivyo vinavyofanywa na serikali kupitia jeshi la polisi  huku wakiitaka serikali kuwaomba radhi waislaam kwa vitendo hivyo ambavyo wameviita ni vya uonevu na udhalilishaji kwa waislam wote nchini.
Mapema leo akizungumza na wanahabari mwenyekiti wa jumuiya hiyo SHEKH MUSSA KUNDECHA amesema kuwa kumekuwa na matukio ya kamata kamata ambayo kwa viongozi wa kiislam,walimu wa madrasa pamoja na watoto ambao wanasoma katika madrasa hizo vitendo ambavyo amesema kuwa vinakiuka haki za binadamu,haki ya kikatiba,kisheria,na utu wa mwislam huku amesema vitendo hivyo vinazidi kuchochea hasira kwa waialam hao na kuhisi kwamba serikali ina mpango wa kuangamiza uislam nchini.
Amesema kuwa vitendo hivyo vinavyoendelea katika mikoa mingi sasa nchini vinazidi kuwagawa watanzania kwa misingi ya dini,na imani zao jambo ambalo amesema kuwa linaweza kusababisha matatizo makubwa kama halitadhibitiwa huku awali.

Akitaja maeneo ambayo kamata kamata hiyo imewathiri waislam wengi ni pamoja na mkoa wa Kilimanjaro ambapo watoto na walimu wa madrasa wamekamatwa,mtwara,kilombero mkoani morogoro ambapo watu waliingia msikitini saa tisa usiku na baada ya muda mchache polisi wakaingia na kuwakamata jambo ambalo amesema bado linawapa shaka kuwa ulikuwa ni mpango uliosukwa.
Naibu katibu mkuu  wa Jumuiya na taasisi ya kiislam Tanzania, Rajab Katimba (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano huo
Amesema kuwa hoja inayoenezwa na serilakali kuwa wanazivamia madrasa kwa kuwa zipo kwenye hali duni na hazina usajili  haina maana kwa kuwa hakuna  sheria inayoonyesha jinsi na vigezo vya kuzisajili huku akisema uduni wa madrasa hizo sio hoja kwani zipo shule hadi wanafunzi wanakalia mawe lakini zimekuwa hazifungi wala kuvamiwa na polisi.
Aidha amesema kuwa kumekuwa na ugumu wa viongozi wao pindi wanapokamatwa na polisi kwa makosa kama hayo ambayo ameita ya kusingiziwa ambapo swala la kuwapatia dhamana limekuwa ni gumu sana na kinachofanyika ni kuwahamisha kutoka kituo kimoja kwenda kingine huku wakiendelea kupatiwa mateso bila makosa ya msingi kutajwa.
Katika hatua nyingine jumuiya hiyo imemtaka mkuu wa polisi nchini IGP,DPP,na kila kiongozi anayehusika na utekelezaji wa matendo hayo kuchukua hatua za kujirekebisha na kuacha kutekeleza uonevu huo dhidi ya waislaam.
Aidha amesema kuwa wao kama waislaam wanaotetea waumini wao wamedhamiria kama ifikapo  tarehe 15 mwezi ujao bila majibu sahihi ya tamkio lao wamedhamiria kufanya maandamano ya amani kuishinikiza serikali kuacha mara moja mpango huo ambao hauna tija kwa waislaam wala taifa kwa ujumla.

No comments: