Sunday, May 17, 2015

CUF--ZOEZI LA UANDIKISHWAJI LIPO HOI,WATANZANIA WENGI WAMEPOTEZA HAKI YAO-SOMA HAPA

 Chama cha wananchi CUF kimesema kuwa ipo hatari ya asilimia kubwa ya watanzania kukosa haki yao ya msingi ya kupiga kura kutokana na wananchi wengi kushindwa kujiandikisha katika daftari hilo kwa sababu ya muda wa kujiandikisha katika zoezi husika kumalizika.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na mwenyekiti wa chama hicho profesa IBRAHIM HAROUNA LIPUMBA wakati akizungumza na wanahabari kuhusu ziara ya kukagua zoezi hilo iliyofanywa na viongozi wakuu wa chama hicho katika mikoa ambayo zoezi hilo linaendeshwa kwa sasa.
Amesema kuwa katika tathmini waliyofanya wamegundua kasoro nyingi ikiwemo wananchi kutokuwa na taarifa za zoezi hilo katika maeneo yao,uandikishwaji kusua sua kwa siku za mwanzo kutokana na wahusika kutokuwa na uzoefu na mashine zinazotumika,hivyo katika maeneo mengi siku saba ambazo ndio zinatumika kuandikisha katika eneo moja hazikutosha hivyo kuna idadi kubwa ya watanzania wamekosa haki hiyo ya kujiandikisha.



Mh LIPUMBA akitolea mfano katika kijiji cha milonde,kata ya matemanga,wilaya ya tunduru asilimia 60 wenye haki ya kuwa wapiga kura hawakupata nafasi ya kuandikishwa katika daftari hilo nkwa kigezo cha siku saba kumalizika hivyo mashine za BVR zimehamishwa ambapo katika idadi ya wapiga kura 2260 waliandikishwa ni 920 tu ambapo tatizo hilo limeonekana katika vituo vingi huku akisema kuwa hali hiyo ni hatari kwani watanzania wengti watakosa haki ya kupiga kura.

Amesema kuwa kutokana na hali hiyo chama cha wananchi CUF kinaiomba serikali kuongeza siku za uandikishwaji kutoka siku saba za sasa hadi kufikia siku 14 kama tume ya uchaguzi ilivyotangaza mwezi wa julai 2014.

Ameongeza kuwa serikali lazima iipe tume ya uchaguzi fedha za kutosha kukamilisha zoezi la kuandikishwa wapiga kura pamoja na serikali kupunguza kupoteza pesa nyingi katika maandalizi ya kura ya maoni na katiba inayopendekezwa kwani kisheria kura hiyo haiwezi kufanyika  kwani sheria ya kura ya maoni imeshavunjwa na hivi sasa hakuna sheria inayoweza kusimamia kura ya maoni.

No comments: