Monday, May 18, 2015

HABARI NJEMA KUTOKA TIGO JUMATATU YA LEO IKO HAPA

 Tigo, kampuni yenye ubunifu zaidi wa kidijitali nchini na EduMe, inayotoa huduma ya  kwanza ya kimataifa ya mambo ya elimu kupitia simu wamezindua bidhaa ya kipekee ya ujasiriamali kwenye simu kwa wateja wa Tigo nchini Tanzania.


Shule ya Biashara inawawezesha watumiaji kujifunza ujuzi wa biashara na ujasiriamali kwa bei nafuu kabisa kupitia  kwenye simu yoyote ya mkononi. Tigo Tanzania, ambayo ni sehemu yakampuni yakimataifa ya mawasiliano  ya  simu na vyombo vya habari ya Millicom, ni ya kwanza barani Afrika kuzindua huduma kama  hii.


Kwa mujibu wa Mkuu wa kitengo cha kidijitali  Bw. Yaya N 'Djore alisema" Kampuni ya Tigo Tanzania ilituzwa ruzuku YA ubunifu kutoka GSMA Connected Women ilikutengene za huduma ya "Shule ya Biashara” mafunzo ya ujasiriamali wa kwenye  simu yanayolenga kuwaandaa wajasiriamali wenye kipato kidogo kuwa na ujuzi unaohitajika kuanza au kukuza biashara "

Somo linatumia hadithi za wamiliki wabiashara wandani na masomo yaliyo chambuliwa ilikutoa mwongozo kwa watumiaji kupitia kila hatua muhimu ya kuanzisha na kuendesha biashara. Masomo yanaelezea mada kama vile, jinsi ya kuchagua wazo la kibiashara, jinsi ya kuongeza uelewa kuhusu biashara na jinsi ya kusimamia biashara yako. Masomo yanatolewa kwa njia ya ujumbe mfupi au sauti kwa lugha ya Kiswahili na kufanya yapatikane kwenye simu yoyote, na kwa watu wenye uelewa mdogo wa lugha ya kiingerezana  au ngazi ya elimu. Baada ya kukamilisha masomo watumiaji wanaweza kupata vyeti vya ujasiriamali vya EduMe-Tigo.

Pia watapata fursa ya kuomba mikopo midogo kupitia kwenye ushirikiano wa Tigo na Benki ya Afrika na Benki ya Wanawake ya Covenant (Tanzania) Ltd.

Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania Bw. Diego Gutierrez, alisema: "Tumefurahi kutoa huduma hii kubwa na mpya kwa wateja wetu. Kuna mahita ji makubwa ya elimu ya biashara nchini Tanzania kwasababu wajasiriamali ndio wanaounda uti wa mgongo wa uchumi wa Tanzania. Kampuni ya Tigo inadhamira ya kukuza maisha ya kidijitali na kubadilisha maisha. Elimu ni muhimu katika hili."

Mkurugenzi Mtendaji wa EduMe Bw.Jacob Waern, alielezea: "Tumefurahi kutoa fursa kwa mamilioni ya watu nchini Tanzania kupata mafanikio katika biashara zao. Dhamira yetu ni kuanzisha huduma mpya za simu zinazohusu elimu ambazo zitawawezesha wateja wetu kujifunza kwa wakati wowote na mahali popote.

Kutokana na kujikita kwao kwenye ubunifu katika masoko ya ndani na dhamira yao ya kutoa huduma tofauti kwa wateja, Kampuni ya Tigo ni mwenza sahihi wa EduMe."

Huduma ya Shule ya Biashara inapatikana kwa wateja wa Tigo. Wateja wanaweza kupata huduma hii kwa kupiga * 148 * 33 # au kwa kutuma ujumbe wenye neon Biashara kwenda 15633.
Ingawa huduma ilifunguliwa kwa watumiaji wachache mwezi Oktoba 2014, huduma mpya ambayo nirahisi kwa watumiaji sasa inapatikana kwa wateja wote wa Tigo. Hadi sasa, Shule ya Biashara ya Tigo imetoa zaidi ya masomo 100,000.Zaidi ya watumiaji 11,000 wameshatumia huduma hii, kati ya hao watumiaji 4,000 niwanawake.

No comments: