Kwa Mujibu wa Taarifa ya NEC kwa Vyombo
vya Habari nchini iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Tumr hiyo Jaji Mstaafu Damiani
Lubuva ambapo inasema kuwa kwa Mujibu wa vifungu vya 35 B (1),(3)(a),37 (1) (a)
na 46 (1),sura ya 343, inaipa Mamlaka
NEC kutangaza Ratiba hiyo.
Pamoja na hayo amebainisha kuwa siku
ya Uteuzi wa Wagombea Urais,Ubunge na
Udiwani utafanyika tarehe 21 Agosti
mwaka huu,
Sanjari na hayo pia
Kampeni za Uchaguzi nazo zitaanza tarehe 22Agosti mpaka tarehe 24 Octoba mwaka
huu,
Ambapo Siku ya kupiga
kura nchi nzima itafanyika tarehe 25 Oktoba mwaka huu.
Kuibuka huko kwa NEC katika kutoa
Ratiba ya Uchaguzi kunakuja Siku Moja kupita baada ya Mwenyekiti wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe kumtaka Jaji Lubuva kuweka bayana
utaratibu wa Uchaguzi ikiwemo siku ya Kampeni pamoja na Tarehe ya kupiga kura.
No comments:
Post a Comment