Thursday, May 21, 2015

TIGO YATENGA SHILINGI BILION 12.6 KUUNGANISHA KANDA YA ZIWA

Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Tigo, John Wanyancha akifafanua jambo kwa wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya ziwa, wakati wa mkutano wao na meneja mkuu wa kampuni ya Tigo Diego Gutierrez uliofanyika jana jijini Mwanza.

Meneja mkuu wa kampuni ya Tigo, Diego Gutierez akifafanua jambo alipoongea na wahariri wa kanda ya Ziwa jana kuhusu jinsi ambavyo Tigo imejipanga kujenga minara mipya 63 katika kanda ya ziwa kwa mwaka huu, wengine pichani (kutoka kushoto) ni CSR Manager Woinde Shisael, Meneja wa Kanda ya Ziwa Ally Maswanya na Territory Manager Joseph Mutalemwa.


   Meneja mkuu wa kampuni ya Tigo, Diego Gutierez akifafanua jambo alipozungumza na wahariri wa kanda ya Ziwa jana kuhusiana na jinsi ambavyo Tigo imejipanga kuwekeza zaidi ya Sh2.6 bilioni katika kanda ya ziwa kwa mawaka huu.
 Kampuni ya simu nza mkononi ya imetenga jumla ya shilingi bilioni 2.6 kwa ajili ya kuwekeza katika ujenzi wa minara mipya na kuboresha utoaji hudumakwa mikoa ya kanda ya ziwa kwa mwaka 2015.

Akiongea na waandishi wa Habari wa mkoa wa Mwanza leo, Meneja mkuu wa kampuni ya Tigo Diego Gutierrez amesema kwamba tigo itajenga minara mipya 63, minara hii itajumlisha minara saba yenye uwezo wa kutoa huduma ya 4G LTE. Kanda ya Ziwa inahusisha jumla ya mikoa nane, mikoa hii ni Mwanza, Shinyanga, Mara, Kigoma, Kagera, Tabora, Geita and Simiyu.

Teknolojia ya 4G LTE inamaanisha kasi na uwezo mkubwa wa kutembelea intaneti na kupakua vitu mbalimbali na pia kupata huduma isiyosumbua ya Skype. Kasi hii pia inawezesha wateja wa Tigo kupata huduma ya video pamoja na mikutano kwa kutumia video (video conferencing), teknolojia hii ambayo tayari kampuni ya Tiggo wanayo, ina kasi mara tano zaidi ya ile ya 3G.

“Kwa mwaka huu tunategemea kujenga minara mipya 63, ili kuwawezesha wakaazi wa vijiji vyote vya mikoa hi inane ya kanda ya Ziwa kupata huduma zetu, kwa wastani tutatumia jumla ya $ 100,000 kwa kila mnara, hii inamaanisha kwamba tuttumia jumla ya dola 6.3 milioni kwa kanda ya Ziwa pekee,” alisema Gutierrez.

“Kwa hili tutakuwa tumewapatia wakaazi wa eneo la kanda ya Ziwa fursa mpya za kijamii na kiuchumi kwa kuwapatia uwezo wa kuona yanayoendelea katika dunia nyingine nje ya maeneo haya, kwa kutumia huduma ya intaneti tutakuwa pia tumewapatia mageuzi ya kidijitali,” aliongeza Meneja Mkuu.
Kwa mujibu wa Meneja Mkuu, Kanda ya Ziwa imekuwa ni eneo ambalo linafaidika zaidi na ufadhili na shughuli mbalimbali za uwajibikaji kwa jamii (CSR) toka kampuni ya Tigo, ambapo imekuwa ikisaidia  jamii katika maeneo ya elimu, afya, mazingira, ujasiriamali, kutengeneza ajira, sanaa na michezo.
Katika miaka miwili iliyopita, Tigo imewekeza wastani wa dola 2 milioni kwa wiki katika mitandao yake hapa nchini. Uwekezaji huu ni pamoja na kupanua wigo wa mitandao kwa kujenga minara mipya hata katika maeneo ya vijijini, kuboresha teknolojia kwa kuleta teknolojia ya 3G ambayo imewezesha wananchi kujipatia huduma ya data, kuwapatia mafunzo wafanyakazi na pia kutekeleza huduma za uwajibikaji kwa jamii (CSR).

Gutierrez pia alisema kwamba katika miezi 12 iliyopita Tigo imewezesha upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi, ikiwa ni pamoja kuwa kampuni ya kwanza nchini kutoa huduma za kimataifa za kifedha zikiwa tayari zimeshawekwa katika viwango vya nchi husika, uanzishwaji wa huduma ya Facebook kwa Kiswahili na pia kuanzisha ushirikiano na watoa huduma wengine ili kuwawezesha wateja kutuma na kupokea fedha kupitia mitandao mbalimbali iliyopo nchini.

Meneja Mkuu aliongeza kwamba mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kuwapatia wateja fursa ya ktoa na kuweka fedha katika akaunti mbalimbali za benki kwa kutumia simu zao za mikononi, kuwapatia wateja gawio la faida kwa kila robo ya mwaka katika akaunti zao za tigo pesa kutokana na salio lililopo, huduma ya muziki kutoka Tigo ambayo inawapatia wateja uwezo wa kupata bila kikomo muziki kutoka sehemu yeyote duniani kupitia Deezer na teknolojia ya 4G ambayo ilizinduliwa mwezi uliopita.

No comments: