Friday, May 1, 2015

VIDEO--KIMENUKA TENA--KIBANDA AWATAJA WALIOMTEKA--CHADEMA WAHUSIKA


Kama unakumbuka lile sakata la kuteswa na kupigwa kwa aliyekuwa mwenyeiti wa jukwaa la wahariri nchini bwana ABSOLUM KUBANDA ambaye alikutana na dhahama ya kutekwa na kuteswa kitendo ambacho kilisababisha sintofahamu kuhusu wale waliomfanyia kitendo hicho.


Sasa sakata hili limeanza kuibuliwa chini chini ambapo KIBANDA akizngumza katika mkutano wa jukwaa la wahariri nchini na chama cha siasa kipya cha ACT-wazalendo alionyesha wazi kuwa anawafahamu waliomfanyia kitendo hicho,kama ukisikiliza vizuri video hii utaskia akionyesha wazi kuwa hakuwa na mahusiano mazuri na viongozi wa chama cha CHADEMA na anakiri kuwa kabla ya kutekwa kwake alikorofishana na viongozi wa chama hicho katika mkutano wa jukwaa hilo na chama hicho mkutano ambao anasema kuwa ulifanyika nyumbani kwa mwenyekiti wa chadema mh FREMAN MBOWE.nakupa nafasi ya kusikiliza na kuitizama video hii kisha uniachie comment zako hapo kama umeelewa alichokizungumza KIBANDA.

No comments: