Thursday, May 14, 2015

WATU WALIOFARIKI DUNIA NA KUTHIBITISHWA KUTOKANA NA MAFURIKO JIJINI DAR ES SALAAM WAFIKIA KUMI NA TATU



Watu waliopoteza maisha jijini Dar es Salaam kutokana na athari ya mafuriko kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha sasa imefikia kumi na tatu. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limethibitisha hilo ambapo mtu mmoja mwanaume aliyetambulika kwa jina la EXAVERY S/O MICHAEL, Miaka 19, Mkazi wa Kingugi Mbagala, alifariki dunia baada ya kusombwa na maji wakati akiwa katika harakati za kuvuka mto Kizinga. 


Tukio hili lilitokea tarehe 13/05/2015 majira ya saa nane kamili mchana huko maeneo bonde la Mto Kizinga Kata ya Kiburugwa Wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam. Maiti yake iliopolewa na wasamaria wema na imehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke kwa uchunguzi na utambuzi.

Nawashukuru wananchi kwa namna wanavyojitolea na kushiriki kushughulikia maafa yanayoendelea kutokea ikiwa ni matokeo ya mafuriko yaliyosababisha na mvua zinazonyesha mfululizo katika jiji la Dar es Salaam.

Nawaomba wakazi wa maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam waendelee kuchukua tahadhali  kwa kuwa madhara zaidi yanaweza kutokea kutokana na kwamba mvua bado zinaendelea kunyesha. Aidha, waendelee kutoa taarifa pindi wanapoona hali yoyote isiyo ya kawaida ili hatua za haraka ziweke kuchukuliwa.
 
S. H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM

DAR ES SALAAM

No comments: