Tuesday, June 30, 2015

MEMBE ALIVYORUDISHA FORM YAKE YA URAIS LEO

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (katikati), akikabidhi fomu za kuomba kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Rajabu Luhavi alipozirejesha katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma jana, baada ya kupata wadhamini wanaohitajika. Kulia ni Mkewe Mama Dorcas Membe.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe (katikati), akizungumza na wanaCCM baada ya kurejesha fomu za kuomba kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), mjini Dodoma jana, baada ya kupata wadhamini wanaohitajika. Kulia ni Mkewe Mama Dorcas Membe na (kushoto) ni Kada wa CCM, Kapteni mstaafu Alhaj Mohamed Ligola.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akikaribishwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Rajabu Ruhavi baada ya kuwasili katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma jana kurudisha fomu za kuomba kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho, baada ya kupata wadhamini wanaohitajika. Picha zote na John Badi

No comments: