Monday, June 1, 2015

NAKUPA HII YA LEO ASUBUHI KUTOKA HUKO TRL--NI MAZINGIRA SAFI

Wafanyakazi wa mamlaka ya reli nchini Tanzania TRL wakiwa katika harakati za usafi mapema leo asubuhi ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya mazingira nchini Tanzania
 Ikiwa dunia inaadhimisha wiki ya mazingira duniani,wafanyakazi wa mamlaka ya Reli nchini Tanzania TRL wameamua kutumia wiki hiyo katika kufanya usafi katika maeneo yote yanayozunguka mamlaka hiyo ikiwa ni njia moja wapo ya kuweka mazingira safi na kuadhimisha wiki hiyo ambayo huazimishwa kila mwaka kwa lengo la kuhamasisha usafi katika mazingira mbalimbali.
Katika shughuli hizo ambazo zilianza leo ndani ya TRL ampayo iliongozwa na viongozi mbalimbali kutoka katika mamlaka hiyo akiwemo Mwenyekiti wa bodi,Mkurugenzi wa TRL na viongozi mbalimbali kutoka shirika hilo linalotoa huduma za usafiri wa reli nchini Tanzania.
Mwenyekiti wa bodi ya TRL Bwana SEVERIN KAOMBWE akizungumza na wanahabari wakati wafanyakazi hao wakiendelea na usafi wa mazingira ya maeneo hayo
Akizungiumza na wanahabari wakati wa shughuli za usafi zikiendelea mwenyekiti wa bodi ya TRL Bwana SEVERIN KAOMBWE amesema kuwa imekuwa ni mazoea kwa watanzania kutokuyathamini mazingira yao kwa kuyafanyia usafi hivyo amewataka watanzania kujua kuwa kitu muhimu katika mazingira yao ni kuyafanyia usafi.
Aidha amesema kuwa ni lazima wafanyakazi hao wajiwekee utamaduni wa kuyafanyia usafi mazingira yao kila siku ili yawe safi na sio kusubiri kipindi cha kuadhimisha siku ya mazingira ndipo wayakumbuke mazingira hayo.
Naye mkuu wa idara ya usafirishaji kutoka TRL Bwana LOLAND SIMTENGU amesema kuwa mamlaka hiyo ipo katika uboreshaji wa mabehewa mbalimbali yanayotumika na abiria ili kuhakikisha kuwa kuna vifaa vya kutosha vya kuweka taka taka ili kuondokana na uchafu kuzagaa wkati wa safari huku akiwataka abiria watakaotumua vifaa hivyo kuwa wazalendo kmuvitunza ili viweze kuwasaidia watanzania wenyewe..PICHA ZAIDI BONYEZA CHINI









No comments: