Tuesday, June 23, 2015

RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AWATUNUKU NISHANI WATUMISHI WA UMMA WALIOLILETEA SIFA TAIFA

N1Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimvisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro Nishani ya Jamhuri ya Muungano Daraja la Kwanza kwa kuwa mwaminifu na kujitolea moja kwa moja kulipatia Taifa sifa kubwa katika Nyanja za kisiasa, kiuchumi, kiulinzi na kijamii wakati wa sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.
N2Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete akimvisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Liberata Rutegaruka Mulamula Nishani ya Jamhuri ya Muungano Daraja la Kwanza kwa kuwa mwaminifu na kujitolea moja kwa moja kulipatia Taifa sifa kubwa katika Nyanja za kisiasa, kiuchumi, kiulinzi na kijamii wakati wa sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.

N3Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete akimvisha Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dkt. Florens Martin Turuka Nishani ya Utumishi mrefu na Maadili mema Daraja la kwanza kwa kuwa mtumishi wa umma kuanzia ngazi ya ukurugenzi na kutumikia Taifa si chini ya ishirini mfululizo na kuonyesha maadili mema wakati wa sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.
N4Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete akimvisha akimvisha Balozi wa Tanzania nchini Burundi Rajabu Hassan Gamaha Nishani ya Utumishi mrefu na Maadili mema Daraja la kwanza kwa kuwa mtumishi wa umma kuanzia ngazi ya ukurugenzi na kutumikia Taifa si chini ya ishirini mfululizo na kuonyesha maadili mema, wakati wa sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.
N5Mwalimu Rosalia Marmo Massay akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete baada ya kuvishwa nishani ya Utumishi mrefu na maadili mema Daraja la Pili kwa kufanya kazi bora na maadili mema yanayostahili kuigwa na wengine kwa muda usiopungua miaka ishirini wakati wa sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.
N6Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete akimvisha CPL Liberatus Tibaitirwa Ndyetabula nishani ya Ushupavu inayotolewa kwa majeshi ya ulinzi na Usalama na watu wengine kwa vitendo vya ushupavu, wakati wa sherehe zilizofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ikulu leo Jijini Dar es Salaam.
N7
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi waliovishwa nishani mbalimbali leo Jijini Dar es salaam.Kushoto ni Jaji MkuuMohamed Chande Othman na kulia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi.
N8
N9Mtoto huyo akimuonesha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete picha aliyoipiga.
N10Mtoto wa Mmoja ya viongozi waliovishwa nishani akipiga picha ya pamoja iliyomjumuisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi waliovishwa nishani
………………………………………………………………………..
Na Hassan Silayo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo amewavisha nishani mbalimbali watumishi wa Serikali kwa kutambua mchango wao kitaifa. 
Rais Kikwete amefanya hivyo kwa kutumia madaraka aliyopewa chini ya sheria ya mamlaka ya Rais (sura ya 9) kamailivyorekebishwa mwaka 2002 fungu la 4 kama ilivyotangazwa katika tangazo la serikali namba 227.

Nishani zilizotunukiwa leo ni Nishani ya Jamhuri ya muungano Daraja la Kwanza, Nishani ya Utumishi mrefu na Maadili mema Daraja la kwanza, Nishani ya utumishi mrefu na Maadili mema Daraja la pili na Nishani ya Ushupavu. 
Nishani hizo zinatunukiwa kwa watumishi ambao sifa zao zimekidhi mmatakwa ya nishani husika 

No comments: