Thursday, August 27, 2015

Kidoogo yatokee mafuriko--Tizama mkutano mzima wa lowasa na wanawake wa Dar es salaam leo



Wanawake kutoka kona mbalimbali za jiji la Dar es Salaam wamejitokeza katika ukumbi wa Milenium Tower katika mkutano wa baraza la wanawake wa Chadema ambao mgeni rasm ni mgombea wa urais wa UKAWA Mh Edward Lowassa ambaye amewataka wanawake kushiriki ipasavyo katika kuleta mabadiliko.


Mheshimiwa Lowassa aliyeambatana na viongozi wa juu wa chama hicho amesema wanawake wana mchango mkubwa wa kufanikisha ndoto za watanzania za kupata mabadiliko ya kweli.
Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa UKAWA akiwemo mwenyekiti wa Chadema Mheshimiwa Freeman Mbowe amewataka viongozi wa UKAWA kote nchini kuhakikisha kuwa wanawake wanapewa nafasi ya kutoa mchango wao ipasavyo.

Awali mke wa mgombea urais kupitia UKAWA mama Regna Lowassa(pichani) amewataka wanawake kuwa mstari wa mbele kuhamasisha jamii kupokea mabadiliko sambamba na kujitokeza kupiga kura na kuhakikisha mabadiliko yanapatikana kwa amani na yanasaidia kupunguza makali ya maisha.






















BOFYA HAPA CHINI UONE PICHA ZA WACHAWI WAKIROGA USIKU

No comments: