Wednesday, August 5, 2015

Team ya ushindi ya ADC hii hapa,aliyetimuliwa CUF kugombea urais mwaka huu

Mgombea urais wa jamhuri ya muungangano wa Tanzania LUTALOSA YEMBA katikati akiwa na mgombea urais wa serikali ya mapinduzi ya zanzibar HAMAD RASHID kulia na kushoto ni mwenyekiti wa chama hicho ambaye sasa ni mgombnea mwenza wa urais bwana SAID MIRAJ wakifurahia mara baada ya mkutano mkuu kupitisha majina yao kukiwakilisha chama hicho katika uchaguzi mkuuu ujao nchini Tanzania
Hamad Rashid Pamoja na Chifu Yemba mara baada ya kuchaguliwa kugombea nafasi za juu ya nchi katika uchaguzi mkuuu ujao

 Wakati vyama mbalimbali viukiendelea kujiweka sawa kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu nacho chama kipya katika uchaguzi huu chama cha ,,,,,,,,,ADC leo kmimetangaza wagombea wake wan a fasi ya urais wa Zanzibar pamoja na mgombea wa urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.


Baada ya mchakato mrefu wa kupitia na kusikiliza hoja za watia nia mbalimbali katika nafasi hiyo mchakato uliopitia katika vikao vyote vya chama hicho  hatimaye mkutano mkuu uliofanyika leo umepitisha jina la chief liemba kuwania nafasi ya urais wa jamhuri ya muun gano wa Tanzania huku jina la mlezi wa chama hicho HAMAD RASHID likipita bila kupingwa kuwania nafasi ya urais wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kupitia chama cha ADC.
 Maadhimio hayo yamefikiwa leo jijini Dar es salaam katika mkutano mkuu wa chama hicho ambapo wanachama walipiga kura ya kuwa na imani na wagombea hao kuipeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mnamo tarehe 25 ya mwezi wa kumi mwaka huu.
Akizngumza na wanachama mara baada ya kuchaguliwa kunai nafasi hgiyo kubwa ya uongozi katika jamhuri ya muungano wa Tanzania chief liemba amesema kuwa ana imani kubwa sana kuwa atafanikiwa kushinda nafasi hiyo huku akitamba kuwa hadi sasa hajaona mgombea kutoka chama chochote nchini ambaye ana uwezo wa kupambana naye katika uchaguzi huo.

 Kiongozi huyo ambaye aliwahi kuwa mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF mkoa wa shinyanga kabla ya kutimkia ADC amesema kuwa ana uzoefu mzuri sana na siasa za Tanzania hivyo hakuna mwanasiasa anayeweza kumsumbua kwa hoja huku akiwaahidi ushindi wanachama na wapenzi wa chama hicho.
Mwenyekiti wa chama cha ADC ambaye sasa ni mgombea mwenza wa urais akizngumza na wanachama wa chama hicho wakati wa mkutano mkuu leo
Naye mgombea wa Urais katika serikali ya mapinduzi ya Zanzibar ambaye hapo awali alikuwa ndani ya chama cha wananchi CUF mh HAMAD RASHID  amesema kuwa sasa Zanzibar  hakuna upinzani kwani chama Tawala CCM pamoja na CUF wameungana na kuunda serikali hivyo chama cha ADC kimekuja kutoa upinzani wa kweli na bhatimaye mwaka huu kufanikiwa kuchukua dola hiyo.


Aidha katika hatua nyingine mgombea urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama hicho chief liembe amemteua mwenyekiti wa chama hicho bwana SAID MIRAJ kuwa mgombea mwenza wa urais katika uchaguzi ujao

No comments: