Wednesday, August 19, 2015

Walimu waipiga mkwara serikali kuelekea uchaguzi mkuu

Rais wa chama cha walimu nchini TANZANIA  Bwana GRATIAN MUKOBA akizungumza na wanahabari mapema leo Jijini Dar es salaam
 Chama cha walimu nchini Tanzania CWT kimeitaka serikali kukamilisha madai ya walimu hadi ifikapo September mwaka huu.
Akizungumza na wanahabari mapema leo Rais wa chama hicho Bwana GRATIAN MUKOBA amesema kuwa serikali imekuwa ikupuuza madai ya walimu hao kwa muda mrefu sasa ambapo amesema kuwa mnamo agost tatu  mwaka huu serikali kupitia wizara ya elimu ilikutana na walimu ili kujadili mambo mbalimbali ikiwemo muundo mpya wa kazi na malipo ya walimu lakini bado serikali haikutoa majibu ya moja kwa moja kuwa itatatua changamoto hizo lini .

Aidha Bwana MUKOBA amesema kuwa sheria ya malipo ya walimu katika kada mbalimbali inaelekeza kuwa mishahara iendane na posho ambapo hadi kufikia leo hakuna posho yoyote iliyotolewa kwa mwalimu yeyote hali inayopelekea deni la walimu kufikia billion tano hadi sasa .

Sambamba na hilo MUKOBA amebainisha kuwa kuna baadhi ya wastaafu ambao hawajalipwa malipo yao tangu mwezi wa nane mwaka jana hali inayowafanya wastaafu hao kubaki omba omba katika maeneo mbalimbali nchini.
Hata hivyo Bwana Mukoba ameongeza kuwa ni lazima serikali itenge hela zinazotosha kulipa madeni yote ya walimu ili kuhakikisha kuwa walimu wanarudisha ari na muamko wa utekelezaji wa majukumu yao ya kujenga taifa na kuboresha mazingira yao ya utoaji wa elimu.



Katika hatua nyingine MUKOBA amesema kuwa mnamo mwezi ujao kutakuwa na mkutano mkuu wa walimu hao ambao pamoja na mambo mengine mada kuu watakuwa wakiangalia serikali imetekelezaje madai hayo waliyoyatoa kabla ya kujadili kwa kina mambo ya kufanya kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

No comments: