Tuesday, September 1, 2015

AMENGOKAA--Dk slaa achafua hali ya hewa upyaaaa,amfumua lowasa na Ukawa yake

KATIBU mkuu wa CHADEMA Dkt Willbroad Slaa ameibuka na kusema aliamua kuachana na CHADEMA na siasa kwa ujumla tangu tarehe 28/08/2015 baada ya Mbunge wa Monduli Edward Lowasa kujiunga na CHADEMA, kwa kile alicho dai kuwa asingeweza kushiriki kumsafisha mtu mwenye madhambi na badala yake aliona ni vyema ajiengue kwakuwa yeye sio muumini wa siasa za ulaghai.
Kauli hiyo ameitoa katika mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, amabapo amesema ameamua kayasema hadharani  kwa kile alicho dai kuna upotoshwaji unao endelea  kuwa yuko likizo na kwamba atajiunga na shughuli za chama hicho mbele ya safari, huku akidai kuwa hakuwa likizo na wala hakupewa barua yoyote ya likizo
Hata hivyo amesema alijaribu mara kadhaa kuandika baraua za kujiuzuru lakini hakuweza kusikilizwa na mtu yoyote, na baadae aliamua kuchukua uamuzi wa kuchana shughuli za chama hicho,  na kwamba uvumi uliokuwa ukiendelea kuwa Slaa amezuiwa na mke wake Josephine
ameongeza kuwa kitendo cha kuwaruhusu baadhi ya wabunge waliotemwa na CCM baada ya kura ya maoni nacho kimechangia kumuondoa katika  chama hicho, huku akimtolea mfano Waziri mkuu wa wazamani Fredrick Sumaye kuwa ndiye mtu ambaye alikuwa na mgogoro nae baada ya kumuita fisadi katika bunge  la jamuhuri ya muungano wa Tanzania, amabapo na yeye leo hii ameendelea kuwaita ni “MAKAPI” .
Naondoka leo huku nikisikitika kuwa sura ya CHADEMA imebadilika nakuwa kama CCM, sasa utawezaje kuleta mabadiliko nawatu wale wale wanaotuhumiwa na kashfa zinao umiza taifa hili? Alisema Dkt Slaa.
Aidha alimaliza kwa kusema amestaafu siasa ila hana chama chochote ila bado ataendelea kuwatumikia watanzania kwa njia nyingine kwakuwa ana vipawa alivyo barikiwa na mungu lakini amewataka wananchi kuto pumbazwa na shamra shamra zinazo endelea badala yake wananchi wanatakiwa kutambua kazi waliyo nayo kwa sasa.
KUHUSU LOWASA KUHUSIKA NA RICHMOND DKT SLAA AME ANIKA HAYA.
kifungu cha 152 cha katiba ya nchi hii kina sema jukumu kubwa la waziri ndio msimamizi wa shughuri za serikali sasa anawezaje kukataa kuwa yeye hakuhusika?
Na katika makampuni yaliyo omba zabuni ya Umeme mwaka 2006, kampuni ya Ricmhond ndiyo kampuni pekee iliyokuwa na sifa “sifuri” haya yoote anayajua na kama hajui basi alikuwa ni mzembe! na kama alikuwa mzembe basi hafai kuwa Rais. alisema Dkt Slaa.
Na aliagiza tenda ifanyike ndani ya siku 10, wakati sheria ya PPRA ina tamka tenda yoyote inatakiwa ifanyike ndani ya siku 45, ni kinyume na sheria.
Sasa hao wanao mtetea watoke hadharani kama mnaona sisi hatujui chochote, mbona mnata kutu pumbaza!?

No comments: