Saturday, September 26, 2015

CHUO KIPYA CHA USTAWI WA JAMII CHAZINDULIWA DAR ES SALAAM

 Na IZACK MAGESA-Dar es Salaam
Taasisi ya isiryo ya kiserikali TASWEP leo imetoa wito kwa jamii nzima kutokujihusisha na vitendo vyovyote vinavyohusiana na maswala ya ukatili wa kijinsia wala unyanyasaji wa aina yoyote katika jamii inatyowanguka.

Wito huo umetolewa leo jijini Dar es salaam na mwenyekiti wa Taasisi hiyo Ndugu NAFUTA RING’ONDI wakati wa uzinduzi wa chuo kipya cha ustawi wa jamii Jijini Dar es salaam ambapo amesema kuwa kuna Haja sasa ya jamii kuepoukana na mfumo Dume kwani ndio chanzo cha vitendo chanzo cha vitendo hivyo vya ukatili katika jamii ambapo ameongeza kuwa chuo hicho kimekuja ili kupambana na na hali hiyo ikiwa ni pamoja na kuongeza elimu ya ustawi wa jamii katika nchi ya Tanzania.
Meneja wa Taasisi hiyo Bi STELLA MNGODO pamoja na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Ndugu NAFUTA RING’ONDI wakishirika katika kukata utepe kuashiria kwa uzinduzi wa chuo hicho kipya cha maswala ya ustawi wa Jamii nchini Tanzania
Aidha akizungumza katika uzinduzi huo meneja wa taasisi hiyo Bi STELLA MNGODO amesema kuwa kwa sasa hapa nchini matatizo ya ukatili wa kijinsia ni mengi ambayo hasa huwakumba zaidi watoto na kina mama hivyo wameamua kufungua chuo hicho ili kupunguza hali hiyo ambapo amesema kuwa chuo hicho mpaka sasa kina wanafunzi 20 wanaosomeshwa bure ambapo kinadhaminiwa na msaada wa watu wa marekani.


Aidha meneja huyo amewataka wanahabari nchini kusaidia jamii katika kuandika na kureport matukio mbalimbali yanayohusiana na jinsia nchini ili kusaidia zaidi katika kupambana na vitendo hivyo

No comments: