Monday, September 14, 2015

wamenasa--Dawa na vipodozi feki vya mamilion vyakamatwa nchini Tanzania

Baadhi ya madawa na vipodozi ambavyo vimekatwa katika operation hiyo
 Mamlaka ya chakula na dawa nchini Tanzania TFDA kwa kushirikiana na jeshi la polisi na shirikisho la polisi kimataifa INTERPOL wamefanikisha kukamatwa kwa dawa na vipodozi haramu vyenye thamani ya shilingi million 135,994,950 .
Ukamatwaji wa dawa hizo na vipodozi haramu ni matokeo ya operation Giboia 2 yenye lengo la kubaini,kukamata na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote wanaojihusisha na biashara dawa bandia,dawa za serikali,dawa ambazo hazijasajiliwa,dawa duni,dawa zilizoisha muda wa matumizi,vipodozi ambavyo havijasajiliwa na vipodozi ambavyo vina viambata sumu.
Mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo  HIITI SILLO  akizngumza na wahabari leo

Akizungumza leo Jijini Dar es salaam na wanahabari kaimu kamishna wa jeshi la polisi mkoa wa Dar es salaam HEZRON GYIMBI ameeleza kuwa maeneo  243 yalikaguliwa wakati wa operation hiyo ikiwa ni maeneo 115 ya Dar es salaam,17 mtwara,13 kilimanjaro,12 arusha,18 mwanza,27 mbeya,na 32 dodoma ikiwahusisha waingizaji  wa madawa famasi za jumla na reja reja,maeneo ya hospitalini,vituo vya afya,maduka ya dawa muhimu pamoja na maduka ya reja reja na jumla ya vipodozi.

Kaimu kamishna wa jeshi la polisi mkoa wa Dar es salaam HEZRON GYIMBI akizngumza na wanahabari mapema leo juu ya zoezi hilo la operaration GIBOIA 2 
Kwa upande wa mamlaka ya chakula na dawa TFDA Mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo  HIITI SILLO amesema kuwa kufanyika kwa operation GIBOIA awamu ya pili ni makubaliano ya mkutano uliofanyika tarehe 9-10 April mwaka huu Harare ili kupiga vita bidhaa bandia na utekelezaji wa maazimio ambayo yalifikiwa katika mkutano huo uliowashirikisha pia  shirika la kimataifa la polisi INTERPOL pamoja na shirika la afya duniani WHO kwa nchi nane zilizopo kusini mwa jangwa la sahara ambazo ni Africa kusini,Zimbabwe,Malawi,Msumbiji,Swazland,Zambia,Angola na Tanzania kwa muda wa siku tatu zoezi ambalo lilifanyika kwa muda wa siku tatu tarehe 19-21Augost 2015.
Wanahabari mbalimbali wakiwa katika kkutano wa utangazaji wa matokeo ya Operation hiyo
Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya chakula na dawa tanzania TFDA,  HIITI SILLO akimuonyesha kaimu kamishna wa polisi Sample ya bidhaa haramu ambazo zimefanikiwa kukamatwa katika zoezi hilo nchini.PICHA ZOTE NA EXAUD MSAKA HABARI
Amesema kuwa kutokana na matokeo ya zoezi hilo hatua mbalimbali zitachukuliwa dhidi ya watu waliokamatwa na makosa hayo ambapo hadi sasa amesema kuwa jumla ya majalada 19 ya kesi yamefunguliwa katika vituo  mbalimbali vya polisi nchini dhidi ya watuhumiwa 


No comments: