Saturday, October 31, 2015

TACCEO WALAANI UVAMIZI WA POLISI KWENYE KITUO CHAO CHA UANGALIZI WA UCHAGUZI

Kaimu Mwenyekiti wa Mtandao wa asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi nchini Tanzania TACCEO ndigu HEBRON MWAKAGENDA akizngumza na wanahabari mapema leo kuhusu uvamizi wa ktuo chao uliofanywa na jeshi la polisi wakati wa mchaguzi mkuu wa Tanzania
 Mtandao wa asasi za kiraia wa kuangalia uchaguzi nchini Tanzania TACCEO umelaani vikali kitendo cha jeshi la polisi kuvamia kituo cha ukusanyaji wa matukio mbalimbali yaliyokuwa yanajili wakati mchakato wa uchaguzi ulipokuwa unaendelea na kuchukua baadhi ya vifaa vya kituo hicho na kuwakamata baadhi ya maafisa wake.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo KAIMU MWENYEKITI WA UMOJA HUO BW HEBLON MWAKAGENDA amesema kuwa tukio hilo lilitokea octoba 29 majira ya saa nane katika eneo la mbezi bichi eneo ambalo kituo hicho kilikuwepo.

Bwana Mwakagenda amebainisha kuwa wakiwa kazini walishuhudia gari ya jeshi ya polisi ambayo ilikuwa na polisi sita waliokuwa wamevaa mavazi ya kujihami pamoja na silaha za moto wakiingia kituoni hapo ambapo askari hao walianza kuchukua vifaa vyao mbalimbali walivyokuwa wanafanyia kazi zikiwemo kompyuta za mezani 25,kompyuta mpakato 3 simu 25 za ofisini na kuwakamata waanglizi wao 36.

Aidha Bwana Mwakagenda ameeleza kuwa matukio ambayo yanafanywa na jeshi la polisi yanatakiwa kulaaniwa na kila mpenda Demokrasia maana yanalenga katika kudhoofisha demokrasia nchini ambayo ndo msingi wa utawala bora
Wanahabari wakichukua Taarifa hiyo
Hata hivyo BW MWAKAGENDA  ameitaka selikali kutotumia vyombo vya dola katika michakato yeyote ya kidemokrasia kwani kwa kufanya hivo kunaweza kuleta uvunjifu wa amani iliyojengwa kwa mda mrefu.

Ameongeza kuwa swala hilo limetokea huku vyombo vya dola vikitambua wazi kuwa uangalizi huo wa uchaguzi ulifwata misingi yote iliyowekwa kikatiba na sheria pamoja na kuwa na vibali na vitambulisho maalum kutoka tume ya uchaguzi vilivyowaruhusu kufanya kazi hiyo kihalali.

Kaimu mkutugenzi wa LHRC ambao ni wataribu wa mtandao huo IMELDA LULU URIO akizungumza katika mkutano huo
Akizngumza na wanahabari katika mkutano huo Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na haki za binadamu nchini Tanzania LHRC ambao ndio waratibu wa mtandao huo Bi IMELDA LULU URIO amesema kuwa tukio la kuvamiwa kwa waangalizi wao na jeshi la polisi sio la kwanza kwani wakati waangalizi hao wakifwatilia zoezi la uandikishwaji wa daftari la kudumu la mpiga kura kwa mfumo wa BVR huko Njombe waangalizi wao walivamiwa na polisi na kupigwa wakiwa katika kazi zao na hadi leo hakuna ufafanuzi wowote uliotolewa na mamlaka husika kuhusu chanzo cha tukio hilo.

No comments: