Thursday, October 8, 2015

VIDEO.---Wazee wa CHADEMA wampongeza KINGUNGE kukihama CCM

Baraza la wazee la chama cha Democrasia na maendeleo CHADEMA leo wamepongeza uamuzi wa kada maarufu na mkongwe wa chama cha mapinduzi KINGUNGE NGOMBALE MWIRU uamuzi wa kukiacha chama chake cha CCM na kujiunga na harakati za watanzania za kusaka mabadiliko huku wakisema ni maamuzi ya kishujaa na yanayopaswa kupongeza na kila mtanzania mpenda mabadiliko.

Akizungumza na wanahabari mapema leo Jijini Dar es salaam katibu wa baraza hilo Bwana RODERICK LUTEMBEKA amesema kuwa maamuzi na kauli alizozitoa mkongwe huyo ambaye anatajwa kuwa ni mmoja wa waasisi wa chama cha mapinduzi ni za kweli na za wazi kwani chama alichokuwepo kinaonekana wazi kuwa kimeshindwa kuwasaidia watanzania na kama mwanasiasa anayeakisi mabadiliko ni hatua sahihi kukihama chama hicho.

Bwana LUTEMBEKA amesema kuwa kauli aliyoitoa kingunge kuwa chama cha mapinduzi kimeishiwa pumzi ni kauli sahihi kwani Chama hicho kimeshindwa kusikiliza na kutatua kero za watanzania huku akisema kuwa chama hicho hakiwezi tena kuepuka mabadiliko ambayo watanzania wengi wanayahitaji kwa sasa.
Ameongeza kuwa watanzania sio siri tena wanahitaji mabadiliko pamoja na hofu kubwa ambayo wamekuwa wakijazwa na vyama vingine kuwa Tanzania haiwezekani bila CCM jambo ambalo amelikanusha na kusema kuwa nchi ya Tanzania inaweza kuendelea kustawi bila uwepo wa CCM ndani ya uongozi wa Tanzania.

Amesema kuwa maneno ya kingunge kuwa chama cha mapinduzi kimeishiwa pimzi lakini ni zaidi ya kuishiwa pumzi ni chama ambacho kinakwenda kufa kutokana na kushindwa kuwahudumia watanzania ambao walikipa dhamana zaidi ya miaka 50 sasa.

No comments: