Tuesday, November 24, 2015

Kilimanjaro Stars Yafufukia challenge,waibamiza Rwanda

Picha na maktaba

TANZANIA Bara imejihakikishia kwenda Robo Fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge baada ya kushinda 2-1 dhidi ya Rwanda katika mchezo wa Kundi A jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Addis Ababa, Ethiopia.

Ushindi huo, unaifanya Tanzania Bara iongoze Kundi A kwa kufikisha pointi sita na mabao sita, huku ikiwa imefungwa bao moja na sasa itamaliza na wenyeji Ethiopia ikiwa ‘haina presha’.
Kilimanjaro Stars leo ilipata bao lake la kwanza kupitia kwa kiungo wa Simba SC, Said Ndemla kwa shuti la mpira wa adhabu dakika ya 22 baada ya Nahodha John Bocco ‘Adebayor’ kuchezewa rafu na mchezaji mwenzake wa Azam FC, Jean Baptiste Mugiraneza.

Winga wa Yanga SC, Simon Msuva na mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara – akaifungia Stars inayofundishwa Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibaden’ bao la pili dakika ya 78.

Rwanda ilipata bao lake la kufutia machozi kupitia kwa Jacques Tuyisenge dakika ya 85. Sasa Amavubi iliyoifunga Ethiopia 1-0 katika mchezo wa kwanza, itamaliza na Somalia waliofungwa 4-0 na Kili Stars.   
 
Kikosi cha Tanzania Bara kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Kevin Yondan, Salum Mbonde, Himid Mao/Jonas Mkude, Simon Msuva, Said Ndemla, John Bocco, Elias Maguri na Deus Kaseke.

No comments: