Sunday, November 1, 2015

LIPUMBA AMERUDI---Tizama alichokisema asubuhi hii mbele ya wanahabari kuhusu uchaguzi mkuu

Mwenyekiti Mstaafu wa chama cha wananchi CUF Profesa IBRAHIM HAROUNA LIPUMBA akisalimiana na wanachama wa chama hicho waliofurika katika makao makuu ya chama hicho asubuhi hii kusikiliza wakati akizungumza na wanahabari leo
STORY NA EXAUD MTEI
 Wakati hali ya kisiasa visiwani Zanzibar ikiwa katika sintofahamu kubwa baada ya uchaguzi kufutwa hatimaye aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF na mwanasiasa mkongwe Profesa IBRAHIM LIPUMBA leo ameibuka na kupinga maamuzi ya kufutwa kwa uchaguzi huo huku akiitaka tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC kuendelea na mchakato wa kumtangaza mshindi wa uchaguzi huo mara moja.

LIPUMBA ameyasema hao leo jijini Dar es salaam katika ofisi za chama cha wananchi CUF Buguruni ikiwa ni mara ya kwanza kwa mawanasiasa huyo kuonekana mbele ya wanahabari tangu kujiuzulu kwake kulikotokana na kutokubaliana na maswala kadhaa ya kisisa yaliyokuwa yanaendelea katika umoja wa katiba ya wananchi UKAWA.
Lupumba Akizngumza na wanahabari kuhusu hali ya kisiasa nchini baada ya uchaguzi
Amesesma kuwa kitendo cha mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar kufuta uchaguzi wa visiwa hivyo na kuitisha uchaguzi mpya ni maamuzi batili kwani kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar na ya Tanzania tume hiyo haina mamlaka ya kufuta uchaguzi hivyo akamtaka mwenyekiti wa tume hiyo JECHA SALUM JECHA kutafakari maamuzi yake ambayo ameyaita ni maamuzi ya kushinikizwa na kisha kuendelea na mchakato wa uchaguzi huo ikiwemo kumtangaza mshindi halali wa uchaguzi huo.

“Ni jambo la kushangaza sana kuona kuwa kura za Zanzibar ambazo zimemuweka magufuli madarakani zinaonekana ni halali laikini uchaguzi wa zanzibari unaitwa kuwa ni uchaguzi batili hii haiingii akilini,haiwezekani pia uchaguzi ulienda vizuri na mwenyekiti huyo alianza kutangaza matokeo ya uchaguzi huo kwa majimbo mbalimbali,lakini baada ya kuona kuwa matokeo hayo yanakiegemea chama Fulani basi amefuta uchaguzi na kuamu kuitisha uchaguzi mwingine hii ni aibu kwa taifa”Amesema mwanasiasa huyo ambaye ni mchumi maarufu Africa.

Lipumba ambaye leo alijitambulisha kama mtanzania mzalendo amemtaka Rais wa sasa wa Zanzibar Dk ALLY MOHAMEID SHEIN kukubali matokeo halali ya kura na kukabidhi nchi kwa mshindi kwani kushindwa kufanya hivyo kutaiingiza nchi hiyo katika machafuko makubwa ambayo yatagharimu roho za wazanzibar kwa ujumla.

Alipoulizwa kwanini kaamua kujitokeza katika kipindi hiki wakati alipokuwa anajiondoa katika nafasi ya uenyekiti wa chama hicho alisema kuwa hatojihusisha katika siasa amesema kuwa amekuwa akiombwa na wanachama na watanzania kutoa ushauri katika sintofahamu hiyo ya uchaguzi hivyo alichokifanya ni kutoa ushauri akiwa kama mtanzania wa kawaida na sio vinginevyo.

No comments: