Monday, December 21, 2015

DR JOHN POMBE MAGUFULI AKUTANA NA MAALIM SEIF IKULU


maa1

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha  Maalim Seif Sharif Hamad ,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Ikulu jijini Dar es Salaam na kufanya  Mazungumzo kuhusu hali ya kisiasa ya  Zanzibar. Katika Mazungumzo hayo viongozi wote wamefurahishwa na hali ya usalama na utulivu inayoendelea.
maa2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Maalim Seif Sharif Hamad ,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Ikulu jijini Dar es Salaam.Rais amemshukuru  Maalim Seif  na amemsihi waendelee na mazungumzo hadi suluhisho la muufaka lipatikane.
maa3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Maalim Seif Sharif Hamad ,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Ikulu jijini Dar es Salaam, wakwanza kushoto ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan.
maa4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha  na Maalim Seif Sharif Hamad ,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan.
7340a1ec-8d32-438e-bc49-8d75870fb164 (1)

No comments: