Saturday, February 6, 2016

PICHA--MAADHIMISHO YA KUTIMIZA MIAKA 39 YA CCM MKOANI SINGIDA


1

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Wananchi na wanahama wa jumbe wa CCM alipowasili Uwanja wa Namfua Mkoani Singida kwa ajili ya kuhudhuria Maadhimisho ya miaka 39 ya CCM leo Februari 6,2016.
2
Katibu Mkuu wa CCM Mhe. Abdulrahman Kinana (kushoto) akizungumza jambo na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Nape Nnauye, kwenye maadhimisho ya kutimia miaka 39 ya CCM iliyoadhimishwa leo Februari 06,2016 katika Uwanja wa Namfua Mkoani Singida, katikati Mhe. Lazaro Nyalandu.

7
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishauriana Jambo na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa waliposimama kwa muda katika kijiji cha Isunna Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida lilipotokea tukio la ajali ya kuanguka gari ya Polisi iliyosabababisha Vifo vya Askari Polisi watatu leo Februari 06,2016.
34
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akikabidhi madawati 1000 kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Paraseko Kone kwenye maadhimisho ya kutimia miaka 39 ya CCM yaliyoadhimishwa leo Februari 06,2016 katika Uwanja wa Namfua Mkoani Singida. Kushoto Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati Mwenyekiti wa CCM Taifa Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.
56
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati, katibu Mkuu wa CCM Mhe. Abdulrahman Kinana kushoto, katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Mkuu wa Mkoa Singida Mhe. Paraseko Kone kulia, wakitoka nje ya Uwanja wa Namfua Mkoani Singida baada ya kuhudhuria maadhimisho ya kutimia miaka 39 ya CCM yaliyoadhimisho leo Februari 06,2016.
1
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu wa awamu ya nne na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Kikwete mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Namfua mkoani Singida kwa ajili ya kilele cha maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM.
2
3
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wanachama wa CCM pamoja na wakazi wa Singida kwenye uwanja wa Namfua waliohudhuria kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM.
6
Rais Mstaafu wa awamu ya nne na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Kikwete akihutubia mamia ya wanachama wa CCM mkoani Singida.
4
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Rais Mstaafu wa awamu ya nne na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Kikwete kulia pamoja na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoani Singida.
5 
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Rais Mstaafu wa awamu ya nne na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Katibu Mkuu wa CCM Abruhamani Kinana.
7
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan pamoja na Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa katika sherehe hizo mkoani Singida.
8
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abrahamani Kinana pamoja na Makamu mwenyekiti wa CCM Taifa Philip Mangula mara baada ya kuhutubia wakazi wa Singida.
9
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya nne na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Jakaya Kikwete wakiondoka mara baada ya kuisha kwa sherehe za kumbukumbu ya kuzaliwa chama cha Mapinduzi CCM Mkoani Singida-
Picha na IKULU
(Picha na OMR)

No comments: