Monday, May 2, 2016

PART 2-Mwenyekiti wa ADC aibuka na mazito juu ya HAMAD RASHID,Aelezea chanzo halisi cha mgogoro ndani ya chama

Mwenyekiti wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC FOR CHANGE -ADC  chenye maskani yake Buguruni SAID MIRAAJ akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam leo
Baada ya jana baadhi ya viongozi mbalimbali wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE ­­-ADC wakiongozwa na Naibu katibu mkuu wake DOYO HASSAN DOYO kuibuka na kumtuhumu mwenyekiti wa chama hicho SAID MIRAAJ pamoja na msajili wa vyama vya siasa kwa kukihujumu chama hicho Hatimaye mwenyekiti huyo ameibuka leo na kueleza mazIto juu ya mgogoro huo ndani ya chama.Anaandika Exaud Mtei kutoka Dar es salaam

Akizunguma na wanahabari leo Jijini Dar es salaam mwenyekiti huyo anayedaiwa kutimuliwa katika nafasi hiyo amesema kuwa mgogoro ndani ya chama hicho umeletwa na mwanachama wa kawaida ambaye ni HAMAD RASHID ambaye amesema lengo lake ni kukitaka kiti hicho cha uenyekiti kinyume na taratibu za chama.

Amesema kuwa tangu kumalizika kwa uchaguzi wa awali visiwani Zanzibar HAMAD RASHID ambaye alikuwa mgombea wa chama hicho Visiwani Zanzibar amekuwa akitoa matamko yanayokihusu chama bila kuwashirikisha viongozi halali wa chama hicho likiwemo tamko la kukubali kushiriki katika uchaguzi wa marudio wa Zanzibar tamko ambalo amesema halikuwa na Baraka za chama hicho.

MIRAAJ amewaeleza wanahabari kuwa yeye kama mwenyekiti wa chama alimpokea  HAMAD RASHID kama mwanachama wa kawaida na baadae kukubali awe mlezi wa chama hicho kutokana na ukongwe wake katika siasa za Tanzania lakini hawakumpa kazi ya usemaji wa chama kwani kwa mujibu wa katiba ya chama hicho msemaji pekee wa chama hicho ni mwenyekiti.

Aidha Ameelaza kuwa kazi pekee ya mlezi wa chama ni kuwashauri viongozi wakuu wa chama na sio kutoa maamuzi ya chama kama aliyoyafanya ya kukubali kurejea uchaguzi wa Zanzibar bila ridhaa ya mwenyekiti na vyombo husika vya chama,huku akimtaka aache kuivuruga katiba ya chama hicho.

Amesema kuwa kwa mujibu wa katiba ya chama hicho baraza la wadhamini la chama halina nguvu yoyote kisheria ya kumuondoa mwenyekiti madarakani kamali livyofanya hivyo yeye ataendelea kuwa mwenyekiti wa chama hicho hadi pale ambapo itaamuliwana na sheria kuwa hafai kuwa mwenyekiti huku akisema anajipanga kwenda kwa msajili wa vyama vya siasa hapo kesho kumweleza masikitiko yake ya kuzuiwa na watu ambao amewaita wahuni ndani ya chama kurejea katika ofisi zake kama kawaida.

Hapo jana Naibu katibu mkuu wa chama hicho DOYO HASSAN DOYO aliwaeleza wanahabari kuwa mwenyekiti huyo haruhusiwi kufika katika eneo lolote la ofisi za chama hadi apate mwaliko maalum wa chama hicho tamko ambalo mwenyekiti huyo SAID MIRAAJ amelikanusha na kusema kuwa limeandikwa kihuni na wahuni wanaotaka kukivuruga chama na yeye hayupo tayari kuwavumilia.

Ameongeza kuwa tamko la chama hicho kwa wanahabari la jana halina uhalali kwa kuwa limeandikwa kihuni bila saini ya mwandikaji,bila jina la mwandikaji hivyo hakuna tamko la chama linalotoka hivyo.
Mgogoro ndani ya chama hicho uliibuka mara tu baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa kwanza wa Zanzibar ambapo swala la uchaguzi wa marudio liliwagawa viongozi hao huku ikionekana wazi kuwa mwenyekiti huyo hakuwa tayari chama cha ADC kushiriki katika uchaguzi huo huku mgombea HAMAD RASHID ambaye ameonekana kuwa na nguvu ndani ya chama hicho kushiriki katika uchaguzi huo uliopelekea chama cha mapinduzi kuibuka na ushindi mnono.

No comments: