Tuesday, May 31, 2016

Taarifa nyingine ya mapokezi ya Zitto na wabunge wa ukawa waliosimamishwa bungeni,wanaanzia Dar


Chama cha ACT wazalendo kinatarajia kumpokea mbunge na kiongozi wa Chama hicho ndugu Zitto Kabwe siku ya JumaaMosi june 4 kwa maandamano yatakayofanyika jijini Dar na kisha mkutano wa hadhara
Pia tayari Kaimu katibu mkuu ndugu Juma Sanani ameshawaandikia makatibu wakuu wa vyama vya Chadema CUF na NCCR-Mageuzi kuwaomba wabunge wao kushiriki katika mapokezi hayo pamoja na mkutano wa hadhara kabla ya ziara hiyo kuelekea mikoani
Jana kamati ya maadili na madaraka ya Bunge iliyoowahusisha wabunge wa CCM iliwafukuza wabunge saba wa vyama vya upinzani kwa sababu ya kusimamia maslahi ya wananchi kuweza kuona mijadala ya bunge moja kwa moja badala ya kuchaguliwa vipindi na serikali ya chama cha Mapinduzi

No comments: