Tuesday, July 5, 2016

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA NISHATI NA MADINI DK. PALLANGYO AJIONEA ZOEZI LA UOKOAJI VIWANJA VYA SABASA

 Ofisa wa Matukio ya Dharura wa Shirika la Madini la Taifa (Stamico), Jeremia Ibambasi (kulia), akitoa maelezo mafupi kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dk Juliana Pallangyo ya uokoaji kwa mtu aliyemeza hewa chafu katika kiwanda cha uchanjuaji dhahabu katika maonesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam 2016 alipotembelea Banda la Wizara hiyo.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dk Juliana Pallangyo (kulia), akiangalia waokoaji wa Shirika la Madini la Taifa (Stamico) jinsi wanavyomsaidia  mtu aliyevuta hewa chafu kwenye kiwanda cha uchanjuaji dhahabu nje ya banda la Wizara ya Nishati na Madini katika maonesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam 2016 katika viwanja vya Biashara vya Mwalimu Nyerere Dar es Salaam leo mchana.
 Hapa mfanyakazi wa Stamico, Paul Thobias (katikati), akionesha jinsi anavyosaidiwa na wataalamu baada ya kuvuta hewa chafu kiwandani.
 Zoezi la kumtoa nguo majeruhi likiendelea. Nguo hizo zinahisiwa huwenda zikawa na hewa hiyo ya sumu.
 Majeruhi akiendelea kutolewa nguo.
 Wananchi wakifuatilia zoezi hilo kwa karibu huku wengine wakiwa wameshika tama.
 Waokoaji wakiondoka na majeruhi wakimpeleka lilipo gari la kubebea wagonjwa tayari kumpeleka mgonjwa Hospitali.
 Hapa  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dk Juliana Pallangyo akiagana na maofisa mbalimbali wa wizara yake baada ya kwisha kwa zoezi hilo la uokoaji.
 Hapa  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dk Juliana Pallangyo akiagana na maofisa mbalimbali wa wizara yake baada ya kwisha kwa zoezi hilo la uokoaji.
 Hapa  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dk Juliana Pallangyo akiagana na Ofisa wa Matukio ya Dharura wa Shirika la Madini la Taifa (Stamico), Jeremia Ibambasi.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

No comments: