Thursday, August 18, 2016

TGNP WAJIVUNIA MAFANIKIO MAKUBWA WA MFUMO WAO MPYA WA URAGHBISHA KATIKA WILAYA SABA WALIZOFIKA

Mkurugenzi wa mtandao wa Jinsia nchini Tanzania TGNP Lilian Liundi akiendesha warsha maalum ya wanahabari iliyofanyika Jijini Dar es salaam kwa lengo la kuwanoa wanahabari kuhusu maswala mbalimbali ya jinsia Nchini Tanzania.
STORY NA VICENT MACHA 
Mkurugenzi wa mtandao wa jinsia nchini Tanzania TGNP Lilian Liundi amesema kuwa mfumo mpya wanaotumia sasa wa kutoa elimu kwa wananchi jinsi gani wanaweza kushiriki katika harakati za kujipatia maendeleo ikiwa ni pamoja na kuwa na uwezo wa kuhoji maswala mbalimbali kwa viongozi wao (Uraghibishi) umefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika wilaya saba walizofanya.

Akieleza zaidi juu ya mfumo huo amesema kuwa  uraghbishi ulianza toka mwaka 2012  na waliweza kuzifikia wilaya saba ambazo ni Kinondoni, Ilala, Temeke, Kisarawe, Mororgoro vijijini,Mbeya vijijini na Kishapu huku  pia wakiweza kuvifikia vikundi zaidi ya 220, wakiwemo wanaume zaidi ya 1000 na wanawake zaidi ya 3000 huku akisema kuwa zoezi hilo linaendelea ili kuwafikia watanzania wengi zaidi.
Ameeleza kuwa njia hiyo imefanikiwa  kusaidia kwa kiwango kikubwa kuweza  kuleta maendeleo kwa kuwa wananchi wengi hawakujua nini wanatakiwa kukifanya endapo serikali imekwama kuwaletea maendeleo.

Akitolea mfano katika maeneo kadhaa maeneo kadhaa amesema kuwa ilikuwa mama mja mzito akitaka kwenda kujifungua inabidi aende na ndoo ya maji kwa kuwa zahanati hazina maji huku  pia mama mjamzito akitakiwa aende na mafuta ya taa au tochi la sivyo atajifungulia gizani. Lakini baada ya kufanya uraghbishi  wananchi wengi walijitoa na kuweza kujichagisha hatimaye kuweza kusogeza huduma karibu kama maji na kupunguza adha ya kwenda na vitu kama mafuta ya taa au ndoo wakati wa kujifungua.
Aidha katika mafanikio mengine ambayo ameyataja yaliyoletwa na njia hiyo iliweza  kufanya kazi kwa baadhi ya maeneo kama shinyanga ambapo palikuwa na shule lakini hakuna vyoo ikasababisha wanafunzi na walimu kuweza kujisaidia vichakani hali ambayo si nzuri kwa afya zao kwani walikuwa wakizalisha magonjwa ya milipuko. Lakini waliweza kuchangishana fedha na kati yao walikuwepo mafundi na wakaweza kupata huduma ya vyoo japo kuwa havikuwa vinatosha lakini viliweza kusaidia ikiwa ni pamoja na mradi wa maji uliowekwa na wana nchi wakisaidiwa na wahisani waliokuwa wakiona adha hiyo kwa wananchi wa maeneo hayo.
Mafanikio hayo ameyataja ikiwa ni ni siku ya pili na ya mwisho  toka warsha maalum ya wanahabari ianze ambayo mtandao wa jinsia Tanzania TGNP uliwakutanisha wanahabari mbalimbali nchini kwa lengo la kuwaelimisha na kutanua uelewa wao juu ya bajeti yenye mlengo wa kijinsia na uraghbishi pamoja na kutilia mkazo au kuhamasisha wananchi kuweza kuhusishwa kwenye upangaji wa bajeti  katika ngazi ya vijiji au kata na mpaka ngazi ya halmashauri na sio viongozi wachache kuwasemea ambapo warsha hiyo iliongozwa na wadau mbalimbali wa maswala ya kijinsia akiwemo mkurugenzi huyo wa TGNP



No comments: