Thursday, September 22, 2016

Kampuni ya Tigo yaendelea na utoaji wa madawati mikoani

Baadhi ya wananfunzi katika shule ya msingi Mandela wakiwa wameketi katika Madawati mapya yaliyotolea na kampuni ya Mawasiliano ya Tigo.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Saidiki akikabidhi Madawati kwa walimu wakuu,Peggy Staki wa shule ya msingi Mandela (kulia) na Peter Njau wa shule ya msingi Mrumeni wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada huo iliyofanyika katika shule ya msingi Mandela mjini Moshi.

Baadhi ya Wananfunzi katika shule ya Msingi Mandela wakiwa wamekaa kwenye Madawati yaliyotolewa na kampuni ya Tigo ikiwa ni kuiikia wito wa rais John Magufuli katika kutekleza sera ya elimu bure. 

Majengo ya shule ya Msingi Mandela. 

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadiki (katikati) akiwa ameketi pamoja na Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Mandela,Peggy Staki (kulia) pamoja na Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Mrumeni Peter Njau ambao shule zao zimepewa msaada wa Madawati 135.

Baadhi ya wageni waliofika katika hafla hiyo. 

Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kippi Warioba (katikati) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa kampunu ya Mawasiliano ya Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata (kulia) na Meneja wa Tigo kanda ya kaskazini ,Henry Kinabo (kushoto). 

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Meck Sadiki akiwa ameketi katika Dawati na Mkurugenzi wa Kampuni ya Tigo Kanda ya Kaskazini ,George Lugata ,katikati ni mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Mandela ,Amina Ally ambayo imepata msaada wa Madawati kutoka kampuni ya Mawasiliano ya simu za mkononi ya Tigo.

Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba akitoa neno la shukrani mara baada ya kupokea msaada wa Madawati 135 kutoka kampuni ya Mawasiliano ya simu za mkononi yaliyotolewa kwa ajili ya shule za msingi za Mandela iliyopo mjini Moshi pamoja na Mrumeni iliyopo wilaya ya Moshi vijijini. 

Wanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Mandela mjini Moshi wakiimba nyimbo za pongezi mara bada ya kupata msaada wa Madawati kutoka kampuni ya Tigo. 

Meza kuu wakifurahia burudani ya nyimbo kutoka kwa wanafunzi wa shule ya Mandela mjini Mosi(hawako pichani). 
 


Sehemu ya Madawati yaliyotolewa na kampuni ya Tigo. 

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiteta jambo na Mkurugenzi wa kampuni ya Tigo,kanda ya kaskazini ,George Lugata. 

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadiki akimweleza jambo Mkurugenzi wa kampuni ya Tigo kanda ya Kaskazini,George Lugata wakati wa hafla ya kukabidhi madawati iliyofanyika katika shule ya msingi Mandela mjini Moshi. 
Picha na Dixon Busagaga.

No comments: