Friday, September 23, 2016

MANENO YA LOWASA BAADA YA KUTEMBELEA WAHANGA WA TETEMEKO LEO

Ijumaa ya Septemba, 23 aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Taifa ya CHADEMA, Edward Lowassa amewasili mkoani Kagera kwa ajili ya kuwajulia hali waathirika wa tetemeko la ardhi ambalo lilitokea Septemba, 10 mwaka huu.Baada ya kuona hali ilivyo sasa kwa baadhi ya wakazi wa mkoa huo kupoteza ndugu zao, nyumba na mali zao kuharibika, Lowassa ametumia ukurasa wake wa Twitter kufikisha ujumbe kwa jamii ya watanzania sehemu yoyote walipo duniani kote.
Ujumbe wa kwanza Lowassa aliandika “Poleni ndugu zangu Wa Kagera na mlioathirika na tetemeko, Tupeane nguvu ili tuvuke katika kipindi hiki kigumu pamoja”
Na ujumbe wa pili Lowassa aliandika “Nawasihi watanzania wenzangu tuendelee kujitolea kuwasaidia wahanga kama ilivyo desturi ya umoja wa kitaifa tulionao”lowassa-kagerall


No comments: