Thursday, September 22, 2016

MTAA WA MASAKI JIJINI DAR ES SALAAM WAANZISHA TOVUTI YAKE KWA AJILI YA MAENDELEO

 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita (kulia), akizungumza katika na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa Tovuti ya mtaa huo iliyofanyika Hoteli ya Best Western Plus Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta. 
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita, akitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya tovuti hiyo.
 Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (katikati), akikata utepe kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kionondoni, aliyekuwa mgeni rasmi, kuashiria uzinduzi rasmi wa tovuti hiyo. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta, Mwenyekiti wa mtaa huo, Kimweri Mhita, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Masaki, Richard Mwakyulu na Mjumbe wa Kamati ya Mtaa huo, Rose Mkisi.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea kabla ya uzinduzi huo.
 Wajumbe wa kamati ya mtaa huo wakishiriki kwenye uzinduzi huo.
 Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo,  Peter Mkongereze akizungumza kwenye hafla hiyo.
 Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta (kulia), akizungumza katika hafla hiyo.
 Mmoja wa waendeshaji wa tovuti hiyo, Benjamin Chaula (kulia), akielezea jinsi itakavyokuwa ikifanya kazi.Kushoto ni Norbert Baranyikwa.
 Makofi yakipigwa baada ya uzinduzi wa tovuti hiyo.
Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.



Na Dotto Mwaibale

SERIKALI ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam imezindua tovuti yake ili kurahisisha mawasiliano na shughuli za maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tovuti hiyo Dar es Salaam leo asubuhi Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Masaki, Kimweri Mhita alisema tovuti hiyo imeanzishwa kwa lengo la  kuwasiliana na kuwashirikisha katika shughuli za maendeleo raia wa kigeni wanaoishi katika mtaa huo.

"Kutokana na jiografia ya eneo letu kulikuwa na changamoto kuwa ya kuwashirikisha wenzetu katika masuala mbalimbali kutokana na kutokuwa na mawasiliano tukaona tuanzishe tovuti yetu itakayosaidia kuondoa changamoto hiyo" alisema Mhita.

Alisema kupitia tovuti hiyo itasaidia kuwatambua wafanyabiashara waliopo katika mtaa huo ambao wameanza kujisajili pamoja na wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, Katibu Tarafa wa Kata ya Magomeni, Fullgence Sakafu alisema kuanzishwa kwa tovuti hiyo katika wilaya hoyo wilaya hiyo mtaa huo umeonesha njia hivyo akaomba mitaa mingine kuiga mfano huo.


Alisema tovuti hiyo itasaidia kuweka wazi mipango ya maendeleo katika mtaa huo pamoja na kuhimizana kwenye kampeni ya kufanya usafi inayoendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuwa.

No comments: