Tuesday, September 13, 2016

TASWIRA MBALIMBALI KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA LEO.

Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. George Simbachawene akitoa taarifa ya serikali kuhusu tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni Mkoani Kagera.
 Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakisimama kwa dakika moja kuungana na wahanga wa tetemeko lililotokea mkoani Kagera
 Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Mhe. Prof. Anna Tibaijuka akichangia hoja kuhusu tetemeko la ardhi mkoani Kagera  wakati wa kikao cha Bunge leo Mjini Dodoma ambapo mbali na mambo mengine wabunge wamekubaliana kuchangia posho ya siku moja kwa ajili ya wahanga wa tetemeko mkoani Kagera.
 Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijini Mhe. John Heche akichangia hoja kuhusu tetemeko la ardhi mkoani Kagera  wakati wa kikao cha Bunge leo Mjini Dodoma

No comments: