Saturday, September 10, 2016

Video-Ombi Maalumu Kutoka kwa Vijana wa ACT WAZALENDO kwenda kwa Rais Magufuli.

Ikiwa Tanzania inaendelea kukabiliwa na kile kinachoitwa Kuminywa kwa Democrasia Hususani kwa vyama vya upinzani kunakodaiwa kufanywa na utawala wa Awamu ya Tano chini ya Mh Jon Magufuli,ambaye amekaririwa mara kadhaa akivitaka vyama vya upinzani kutokufanya siasa hadi ifike mwaka 2020 kwa maelezo kuwa sasa ni muda wa kazi sio siasa.

Vyama vya upinzani vimeendelea kupingana na maagizo hayo huku wakieleza kuwa ni kinyume na katiba ya nchi.
Ngome ya vijana ya Chama Cha ACT-WAZALENDO ni miongoni ya wanaopinga maagizo hayo huku wakidai kuwa maagizo hayo yapo nje ya katiba na hayawezi kutekelezwa.

Edna Sunda Ni Katibu wa ngome hiyo ya vijana Hapa ameamua kutuma Ombi maalum kwa Rais wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli unaweza kutizama video hii

No comments: