Tuesday, November 15, 2016

Lowasa hakuonekana kwenye msiba wa Sitta na Mungai,ametolea Ufafanuzi Taarifa hizo


Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametoa ufafanuzi kuhusu kutoonekana kwake kwenye misiba ya viongozi wawili wa zamani serikalini, Samuel Sitta na Joseph Mungai.

Sitta, aliyekuwa Spika wa Bunge la Tisa, alifariki dunia Novemba 7, akiwa Ujerumani alikokwenda kutibiwa tezi dume na siku iliyofuata alifariki Mungai, aliyekuwa Waziri wa Elimu wa Serikali ya Awamu ya Tatu.
Gumzo kwenye mitandao ya kijamii lilikuwa ni kutoonekana kwa Lowassa, ambaye hivi sasa ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema.
Lowassa alisema kuwa, kilichomkwamisha kufika kwenye misiba hiyo ni kuwa safarini Afrika Kusini alikokwenda kumuangalia mdogo wake, Bahati Lowassa aliyekuwa mgonjwa.

No comments: