Sunday, November 6, 2016

MSIBA MKUBWA TANZANIA-SAMWELI SITTA HATUNAYE

Aliyekuwa Spika mstaafu wa Bunge na Waziri Mwandamizi Mhe. Samuel Sitta amefariki dunia usiku wa kuamkia leo huko Ujerumani akiwa katika matibabu. 
Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo husika vinaeleza kuwa Mzee Sitta amepatwa na umauti huo katika hospitali nchini Ujerumani majira ya saa 7:50 kwa  muda wa Ujerumani.
Mtandao huu utaendelea kuwaleteaa habari kamili kila zitakapotufikia
Poleni ndugu , jamaa na marafiki wote na Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahala pema peponi.
CREDIT MO BLOG

No comments: