Friday, November 4, 2016

SIMU YA AINA YAKE YAZINDULIWA DAR ES SALAAM,NI THURAYA,INATUMIA SATELLITE KATIKA MAWASILIANO YAKE

Simu hizo za THURAYA  zinazotumia mawasiliano ya Satellite 
 Hii inaweza kuwa ya kwanza kutokea kwa Tanzania katika kumbukumbu za maswala ya mawasiliano hususani ya simu za mkononi ambapo Jana Jijini Dar es salaam imezinduliwa Simu ya aina yake ambayo tofauti na simu za kawaida simu Hii inatumia Mawasiliano ya njia ya SATELLITE ambayo ni tofauti na simu nyingine ambazo zinatumika nchini kwa sasa ambazo zinatumia Mtandao wa njia ya kawaida wenye minara ya Baharini.
Meneja Mauzo wa kampuni hiyo kwa Africa  Augustus Kamitu Akitoa maelezo mbalimbali kwa watanzania waliofika katika uzinduzi wa Simu Hizo moya nchini Tanzania zinduzi ambao Ulifanyika Jijini Dar es salaam Jana na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wakiwemo wanahabari na wadau wengine.


THURAYA XT-PRO ni moja kati ya simu Bora sana Duniani kwa sasa zinazotumia Satellite ambayo pia inasifika kuwa na uwezo mkubwa wa Vifaa vyake kama Battery,na uwezo mkubwa wa Mtandao bila kujali eneo ulilopo kote duniani,sifa nyingine kwa simu hiyo ni pamoja na kuwa na Kioo imara cha simu yake chenye uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya aina yoyote
Wadau Mbalimbali wakikagua simu aina ya Thuraya ambazo zimezinduliwa Jana Jijini Dar es salaam
Katika uzinduzi wa Thuraya XT-PRO Jana Jijini Dar es salaam Meneja Mauzo wa kampuni hiyo kwa Africa  Augustus Kamitu amesema kuwa kupitia simu za Thuraya XT-PRO mtumiaji atakuwa na uwezo wa Kupiga simu na kupokea simu pamoja na kutuma messege kwa kutumia Satellite ikiwa ni pamoja pia na kutumia mtandao kufanya shughuli mbalimbali pamoja na mitandao ya kijamii kwa Kutumia Mtandao wa satellite.
Bwana Roen Evan Manezes  ambaye ni Mkurugenzi wa mauzo wa kanda ya Kati mashariki na africa akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo wanahabari na wadau wa mawasiliano wakati wa Uzinduzi wa Thuraya simu zinazosifika katika Kutumia Satellite Duniani


Ameongeza kuwa ubora wa Thuraya unajidhihirisha zaidi pale ambapo ukiwa na simu hiyo hutakuwa na hofu ya eneo ulilopo kwani simu hizo zina uwezo wa kuhimili mtandao eneo lolote ulilopo bila kuwa na usumbufu wa mtandao

Simu hizo kwa sasa zinapatikana zaidi ya mataifa 160 ya dunia nzima ikiwemo Ulaya,Asia,Africa na Australia ambapo kwa Tanzania imezinduliwa Jana Jijini Dar es salaam na kwa sasa inaoatikana.










No comments: