Wednesday, November 9, 2016

Umeme wa megawati 1,200 utaongezwa katika gridi ya taifa kusaidia kukabili uhaba mkubwa wa umeme Tanzania

Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Bima ya Biashara Afrika (ATI) George Otieno akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa mkutano maalum uliofanyika Jijini Dar es salaam kwa lengo la kuwaeleza wanatazania juu ya kinachojadiliwa katika mkutano wa jukwaa la kimataifa la sekta ya nishati  ambalo likiwa na kauli “Kufungua uwekezaji kutawezesha ongezeko kubwa la Nishati Tanzania” ambalo limeitishwa na ATI mkutano ambao Unafanyika Jijini Dar es salaam.PICHA ZOTE NA EXAUD MTEI HABARI24 BLOG

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umeme Tanzania TANESCO  Dr Deckisn Mhaiki akizungumza na wanahabari hao wakati wa kueleze aushiriki wa Tanesco katika mkutano huo  unaofanyika Jijini Dar es salaam  Mkano ambao ni mkutano wa jukwaa la kimataifa la sekta ya nishati  

Msajili wa Hazina ofisi ya hazina Laurence Mafuru akizngumza na wanahabarin ambapo amesema kuwa Serikali imejipanga kuwatengenezea wawekezaji nhasa wa maswala ya Nishati mazingira mazuri ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na Bima nzuri na ndio maana serikali imeingia Ubia na wakala hao wa Bima kwa ajiji ya kuboresha huduma huzi Tanzania.

Tusekile Kibonde ambaye ni Underwritter Responzible for Tanzania Kutoka ATI akieleza maswala mbalimbali mbele ya wanahabari juu ya Mkutano huo ambao unafanyika Jijini Dar es salaam ambapo Jukwaa hilo linawakutanisha  pamoja  wadau kutoka Nyanja binafasi za za umma  katika kutafuta masuluhisho   ambayo yataondoa hatari  zinazoikabili sekta ya nishati ili kuvutia  uwekezaji unaohitajika sana.

Commissioner General Tanzania Insuarance Regulatory authority and Board chairman  Israel Kamuzora akizungumza katika mkunao huo wa wanahabari.


Mwenyekiti wa wa wakala wa umeme Vijijini Dr Gideon Kaunda akizungumzia umuhimu wa jukwaa hilo ambalo limekutana Jijini Dar es salaam

Katika mkutano wa waandishi wa habari leo Wakala wa Bima ya Biashara Afrika (ATI) umeitaka serikali ya Tanzania  kuimarisha ushirikiano uliopo baina yake  hivi sasa ambao utawezesha wakala huyo  kuingia  uwekezaji mkubwa wa dola za Marekani bilioni 1.2 (2.6tr/-) katika sekta ya nishati  pamoja na nyongeza ya megawati 1,200 katika gridi ya taifa.


Tanzania ni mmoja wa wajumbe waliasisi ATI wakala ambao ulianzishwa ili kutoa  bima kwa wawekezaji  pamoja na kufanya shughuli nyingine za kibiashara miongoni mwa nchi za Afrika ambazo ni wanachama. Chini ya ubia am,bao ulisainiwa na Rais Mstaafu Mheshimiwa Benjamini William Mkapa mwaka 2001, Tanzania na nchi nyingine  zilikubaliana  kutoa upendeleo wa kupata mkopo   katika miradi yote inayoungwea  mkono na ATI. Ahadi hiyo ambayo inatoa uhakika kwa nchi mwanachama  ambao utaiepusha na madai yoyote  katika miradi inayoungwa mkono na ATI, kuwapatia wawekezaji, wagavi na  na nafasi nyingine muhimu katika kuzindua miradi Tanzania.

“Lengo letu ni kuisaidia Tanzania  kwa kuuleta nchini uwekezaji  unaohitajika sana  na kupunguza  gharama za kukopa. Sisi ni watu wakimya  lakini ni sehemu muhimu sana ya fumbo  kwa sababu tumesimama nyuma ya uwekezaji na biashara ambayo  inakadiriwa kufikia dola bilioni (2tr/-) nchini Tanzania  tangu kuanza kwa  biashara mwaka 2004”, alibainisha Ofisa Mtendaji Mkuu wa ATI George Otieno.

Tanzania inaweza kunufaika zaidi kutokana na ubia wake na ATI kirahisi kwa kurudia utekelezaji wa ahadi zake  kwa kusaidia miradi  inayoungwa mkono na ATI ndani ya Tanzania. Chini ya masharti ya ubia, Tanzania  inaweza  kuwepo kiwango mbadala wa vipimo vya viwango kwa kipimo cha uwekezaji cha ATI daraja A mara tutakaposaini  manunuzi yanayoungwa mkono na ATI. Chini ya kanuni za Basel, ambazo zinasimamia mabenki mengi ya kimataifa, ynaweza kuikopesha nchi  kama Tanzania  ikiwa inaungwa mkono katika bima na taasisi kama ATI,  ambayo ni taasisi inayoheshimika na  inayoaminiwa na masoko ya kimataifa ya fedha. Bima ya ATI  inaiwezesha benki kupunguza kiwango cha mwisho cha malipo ya bima, ambacho kwa kiwango kikubwa kinapunguza  gharama za kukopa kwa Tanznaia na nchi nyingine za Afrika ambazo ni wanachama.

Kushindwa kutumia kikamilifu  fursa hii, Tanzania inaweza kukosa uwekeza wenye  thamani ya mamilioni ya fedha. “ATI  inaweza kuisaidia nchi kuwa inavutia kuwekeza kifedha  kwa kuvutia uwekezaji zaidi. Hili ni muhimu hususani katika sekta ya nishati  ambayo kwa hivi sasa ina ushindani mkubwa,” alisema Mdhamini Mkazi wa ATI nchini Tanzania  Tusekile Kibonde.


Mkutano huo wa waqandishi wa habari umefanyika  wakati mkutano wa jukwaa la kimataifa la sekta ya nishati  ambalo likiwa na kauli “Kufungua uwekezaji kutawezesha ongezeko kubwa la Nishati Tanzania” ambalo limeitishwa na ATI. Jukwaa hilo linawakutanisha  pamoja  wadau kutoka Nyanja binafasi za za umma  katika kutafuta masuluhisho   ambayo yataondoa hatari  zinazoikabili sekta ya nishati ili kuvutia  uwekezaji unaohitajika sana.

Wakala wa Bima ya Biashara Afrika (ATI) ulianzisha zaidi ya mwongo mmoja uliopita  na Tanzania na nchi nyingine wanachama wa Soko la Pamoja na nchi za Kusini mwa Afrika (COMESA), Benki ya Dunia (WB), na Benki ya hivi karibuni ya Maendeleo Afrika (ADB) ili kusaidia  kuvutia uwekezaji kutoka nje (FDI) na kusaidia biashara. ATI inashughulikia masuala yanayowahusu wawekezaji  kwa  kuzipatia bima  biashara zao dhidi ya majanga mbalimbali za kiuwekezaji  kama vile kushindwa kuilipa serikali au wakala wa serikali. Hali kadhalika ATI inazilinda kampuni za ndani  zinazovutiwa  katika kupanua biashara zao ndani ya masoko mapya. ATI  ilianzishwa uwepo katika maqzingira ya ndani nchini Tanzania mwaka 2010. Taasisi ya Sekta  Binafsi Tanzania (TPSF) ndio  mwenyeji wake  katika ofisi yake ya Tanzania.

Nchini Tanzania ATI inaunga mkono sekta  binafsi na serikali katika kushughulikia  changamoto katika nishati, mawasiliano ya simu  na huduma za kifedha. Katika sekta ya nishati ATI inaisaidia kampuni  ya Norway ambayo imepewa ukandarasi na serikali  katika kujenga vituo vya umeme na hali kadhalika  kiasi cha dola milioni 62 (132bn/-) kwa ajili ya kuwezesha kujengwa  kwa kuanzisha ushirika na mabenki  kwa ajili ya matumizi ya serikali. Kutokan ana uungwaji mkono huo wa ATI katika  miradi kama hiyo , Tanzania imeweza  kuingiza mega wati 400 za umeme za ziada katika gridi ya taifa.

No comments: