Monday, December 26, 2016

NAPE,MBOWE WAONGOZA KUUAGA MWILI WA MPOKI BUKUKU DAR

 Wanahabari wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mpigapicha Mwandamizi wa The Guardian, marehemu Mpoki Bukuku baada ya kutolewa heshima za mwisho katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Tabata, Dar es Salaam, tayari kulisafirishwa kwenda kwao Msalato Dodoma kwa mazishi. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akiwaongoza waombolezaji kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Mpigapicha Mwandamizi wa The Guardian, marehemu Mpoki Bukuku katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Tabata, Dar es Salaam. Mwili wa Mpoki ulisafirishwa kwenda kwao Msalato Dodoma kwa mazishi.
 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman  akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa mpendwa wetu Mpoki Bukuku

 Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa akiwa ameshika shada la maua alipokuwa akiingiza kwenye gari lenye jeneza la mwili wa marehemu Mpoki Bukuku
 Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo ambaye pia ni Mmiliki wa Blog hii, Richard Mwaikenda akitoa salamu za rambirambi za Chama cha Mabloga Tanzania (TBN) wakati wa kuaga mwili wa mpendwa Mpoki Bukuku.
 Mwakilishi wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo  vya Habari Habari Tanzania (MOAT), Saed Kubenea akitoa salamu za rambirambi
 Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile akitoa salamu za rambirambi
 Mwakilishi wa Chama cha Wapigapicha za Habar Tanzania (PPAT), Selemani Mpochi akitoa salamu za rambirambi. Mpoki alikuwa mwanachama wa chama hicho.
 ADMIN wa Group la WhatsApp la Tasnia, Thomson Kasenyenda akita salamu za rambirambi na kuahidi group hilo kuwasilisha mchango wao kwa kulipia ada za shule za watoto wa marehemu
 Mwenyekiti wa Chama cha Bongo Movie, Steven Nyerere akitoa salamu
 Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo na Burudani Tanzania (TASWA), Juma Pinto akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Mpoki Bukuku.
 Benny Kisaka akitoa heshima za mwisho
 Mhariri Mtendaji wa The Guardian, Mgamba akitoa heshima za mwisho
 Mmiliki wa Blog ya Michuzi, Muhidini Issa Michuzi akitoa heshima za mwisho
 Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa mpendwa wao Mpoki Bukuku

 Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete akitoka kutoa heshima za mwisho

 Mpigapicha wa The Guardian na Nipashe akisaidiwa baada ya kutoa heshima za mwisho
 Mpigapicha wa zamani wa Daily News, Athuman Khamisi akitoa heshima za mwisho
 Mtoto wa kike wa maraehemu Mpoki Bukuku akimvalisha Rozali wakati wa kuaga mwili wa babake
 Mjane wa marehemu Lillian  akiubusu mwili wa mumewe
 Mtoto wa kiume wa marehemu Mpoki Bukuku, Junior akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa babake

Jeneza lenye mwili wa mpendwa wetu Mpoki Bukuku likiingizwa kwenye gari tayari kwa safari ya kwenda Msalato Dodoma kwa mazishi.

No comments: