Wednesday, February 1, 2017

Diwani wa Kata ya Ndugumbi Mh Thadei Massawe akabidhi Vyeti kwa Madereva Pikipiki (Bodaboda ) waliokuwa katika mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo

Diwani wa kata ya Ndugumbi Mh Thadei Massawe(Katikati) Pamoja na Afisa Kata wa ndugumbi wakimkabisho mmoja kati ya madereva 27 wa pikipiki Maarufu kama Boda Boda cheti maalum cha kuashiria kumaliza mafunzo ya siku kumi yaliyokuwa yanatolewa na serikali kupitia Kata hiyo,Mafunzo yakiyokuwa na lengo la kuwajengea uwezo madereva hao juu ya kazi yao na kuwakinga na ajali za barabari pamoja na Athari nyingine nyingi za kazi hiyo.

Picha ya Pili na ya tatu zikimuonyesha Mwenyekiti wa Madereva wa Madereva wa Pikipiki Mkoa wa Dar es salaam Bwana Michael Massawe ambaye katika shughuli Hiyo alimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Paul Makonda.

Ambapo akizungumza kwa Niaba yake amesema kuwa Mkoa wa Dar es salaam umejipanga kuhakikisha kuwa unawapa uwezo mkubwa madereva wa pikipiki ili waweze kufanya kazi zao kwa ustadi zaidi na kuepuka ajali na majanga ambayo yanaweza kuzuilika kwa urahisi,Amesema kuwa mafunzo kama hayo ambayo yamehitimishwa leo Katika kata ya Ndugumbi ni Mpango wa Serikali kupitia Trafic kikosi cha usalama Barabarani kuhakikisha kuwa madereva wanapatiwa elimu na kuwa na leseni zinazowafanya kuendesha Vyombo Hivyo bila madhara yoyote

Diwani wa kata ya Ndugumbi Mh Thadei Massawe akizungumza na madereva hao 27 waliohitimu mafunzo hayo ambapo amewata kuhakikisha kuwa wanazingatia kile ambacho wamejifunza kwa siku hizo kumi huku akisisitiza kuwa endapo watafwata waliyofundishwa ana uhakika kuwa kutakuwa na kupungua kwa Ajali za bodaboda na matatizo ya ujambazi wa piki piki katika kata yake
Baadhi ya Madereva waliohitimu mafunzo hayo leo Jijini Dar es salaam katika kata ya Ndgumbi




No comments: