Sunday, March 26, 2017

COVENANT BENKI KUKISAIDIA KIKUNDI CHA FARASI KUNUNUA HISA ZA VODACOM NA KUWAPATIA BIMA YA AFYA KWA WANA KIKUNDI

Covenant ni benki inayowajali wananchi wa hali ya chini na idara binafsi. Leo kikundi hiki cha farasi kimeweza kutimiza mwaka mmoja. Kikiwa ni kikundi kilichoweka fedha zake katika benki hiyo na kuweza kupewa mwongozo jinsi ya kunufaika na huduma za benki hiyo. Wanachama wa kikundi hiko walianza wakiwa 20 na na kwa sasa wapo 40 na bado kuna wengine wanaomba kujiunga. Grace Boniphace Luwiku Mwenyekiti wa kikundi hiko alisema kuwa wanafurahia mafanikio ya mwaka mmoja wakiwa ndani ya Covenant kwa kuwa waliweza kutimiza malengo yao waliyo ya kusudia. walihitaji kuwa na biashara ya pamoja waliweza kufanikiwa na walihitaji kila mwanachama awe na biashara yake waliweza pia na waliona kitu muhimu ni afya waliweza kukatiwa bima ya afya  ya AAR.
Na kwa leo wanaweza kufurahia mafanikio waliyoyapata ndani ya mwaka mmoja.

MKURUGENZI MTENDAJI WA COVENANT BENKI SABETHA MWAMBENJA AKIONGEA NA VYOMBO VYA HABARI  KWA  KUKIPONGEZA KIKUNDI CHA FARASI KUTIMIZA MWAKA MMOJA.
Mkurugenzi mtendaji wa Covenant benki Sabetha Mwambenja aliweza kuwapongeza kwa kutimiza mwaka mmoja. Na kuweza kutimiza sehemu kubwa ya malengo yao ikiwa hivi karibuni wanafungua mgahawa wa chakula na vitu vingine mbalimbali. lakini pia wao kama benki waliweza kuwasaidia kununua hisa za  kampuni ya Vodacom. Na kitu kingine aliweza kuwasifu kwamba wao hawavunji tofauti na vikundi vingine wanaweka pesa zikiwa nyingi wanavunja na kugawana. lakini hawa wako tofauti kwa kuwa wao wanakopeshana ndani ya kikundi na mtu anarudisha kwa riba na baadae pesa inayopatikana wanagawana kama faida. Hii inaweza kuwasaidia kwa benki kuweza kuwaamini na kuwapa huduma nyingine kubwa ikiwemo mikopo mikubwa ya kujiendesha wenyewe ndani ya kikundi.

MWENYEKITI WA KIKUNDI CHA FARASI AKIELEZEA MAFANIKIO WALIYO YAPATA NDANI YA MWAKA MMOJA WAKIWA CHINI YA COVENANT BENKI.

BAADHI WANACHAMA WA KIKUNDI CHA FARASI GROUP WAKIWA KATIKA KUSHEREHEKEA WALICHOKIVUNA NDANI YA MWAKA MMOJA WA KIKUNDI HIKO.

NA MWANDISHI WETU VICENT MACHA.

No comments: