Monday, April 24, 2017

JOKATE MWEGELO AANZA JUKUMU UVCCM,TIZAMA WALICHOSEMA LEO

 Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) leo umefanya mkutano na waandishi wa habari lengo likiwa ni kujadili mustakabadhi wa nchi yetu na mambo mbalimbali yanayohusu umoja huo.
      Uvccm wamepongeza jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali kwa kuweza kudumisha muungano. Lakini pia wamepongeza wananchi wa pande zote mbili ikiwemo Tanzania bara na Tanzania Visiwani kwa kuendelea kuenzi muungano huo tangu hapo mwaka 1964 mpaka hivi sasa. Ikiwa kuna mataifa mengi yalijaribu kuungana lakini muungano wao haukuweza kudumu na  kwetu sisi ni jambo la kujivunia kwa hivi kesho kutwa  kuweza kutimiza  miaka 53 ya muungano huo. Lakini pia wametoa wito kwa vijana wa Dodoma na maeneo ya karibu  kuondoa tofauti ya vyama na usiasa na kujitolea kuungana kushiriki katika maadhimisho hayo ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya taifa letu kuweza kufanya maadhimisho  katika mji wa Dodoma.   Inafaamika kuwa UVCCM ni jiko pia ni tanuru linalowapika vijana kuja kuwa warithi wazuri wa selikali na kisiasa. Kufuatia hili umoja huo umeweza kufanya mabadiliko ya baadhi ya nafasi kutokana wakuu wa idara wengine kuweza kuteuliwa kuwa makatibu wakuu CCM wa wilaya hivyo kuacha baadhi ya nafasi wazi. Kamati ya utekelezaji UVCCM taifa ilikutana katika kikao chake kilichofanyika upanga Dar es salaam tarehe 18/4/2017 iliweza kuteua wajumbe wake kama ifuatavyo.
Doris H. Obeid – idara ya uchumi uwezeshaji na fedha
Daniel M. Zenda – Idara ya vyuo na vyuo vikuu
Jokate U. Mwegelo – Idara ya uamasishaji na chipukizi
Mohamedi  A. Abdalah – Idara ya organization, siasa na uhusiano wa kimataifa
Islael sostenes   - Idara ya usalama na maadili
        Pia umoja huo umekemea vikali kitendo kinachofanywa na gazeti la Tanzanite kupitia machapisho yake ikiwa la tarehe 10 – 16 lenye kichwa kinachosema “UVCCM isafishwe “ na toleo lake la tarehe 24 – 30 lenye kichwa ” kashfa nzito UVCCM “  umoja huo wa vijana unamuomba muhariri wa gazeti hilo kuomba radhi mapema kabla hatua stahiki hazijachukulia dhidi ya gazeti hilo kwani kitendo hicho ni kudhalilisha umoja wa Vijana CCM na kuwafanya wananchi wasiwe na imani na umoja huo.


No comments: