![]() |
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Ashatu Kijaji akizungumza na wanawake wajasiriamali 1,500 waliohudhuria hafla ya KCB 2jiajiri Malkia wa Nguvu. Naibu Waziri aliipongeza Benki ya KCB kwa kutambua mchango wa mwanamke katika jamii na kuanzisha program ya KCB 2jiajiri inayo lenga kutatua changamoto zinazo wakabili wanawake wajasiriamali Tanzania. |
|
![]() |
Mkurugenzi wa vipindi wa Clouds Media Group, Bw. Ruge Mutahaba akizungumza na wanawake wajasiriamali 1,500 waliohudhuria hafla ya KCB 2jiajiri Malkia wa Nguvu. |
![]() |
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya KCB Bw. Masika Mukule akizungumza na wanawake wajasiriamali 1,500 waliohudhuria hafla ya KCB 2jiajiri Malkia wa Nguvu.
|
![]() |
Waziri wa Biashara na Viwanda- Zanzibar Mhe. Amina Salim Ally akizungumza na wanawake wajasiriamali 1,500 waliohudhuria hafla ya KCB 2jiajiri Malkia wa Nguvu.
|
![]() |
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa benki ya KCB Bi. Christine Manyenye akizungumza na wanawake wajasiriamali 1,500 waliohudhuria hafla ya KCB 2jiajiri Malkia wa Nguvu. |
Dar es Salaam, AprilI 6, 2017. Benki ya KCB Tanzania iliendesha tamasha la KCB 2jiajiri Malkia wa Nguvu jijini Dar es Salaam kwa wajasiriamali ambao ni wanachama wa KCB 2jiajiri pamoja na wasio wanachama. Tamasha hilo lilifanyika katika ukumbi wa King Solomon na kuhudhuriwa na wanawake wajasiriamali zaidi ya 1,500 ambao walisherehekea, kuonesha bidhaa zao na kuunda mitandao ya kibiashara ili kukuza masoko yao.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dr. Ashatu Kijaji, na Waziri wa Biashara na
Viwanda – Zanzibar Mhe. Amina Salim Ally, Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya KCB
Bi. Zuhura Sinare Muro na wajumbe wengine wa bodi ya KCB.
Akizungumza katika tukio hilo
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya KCB, Masika Mukule alisema kwamba “Hafla
ya KCB 2jiajiri ni muendelezo wa programu ya KCB Bank kuwawezesha wanawake
wajasiriamali (women empowerment/capacity building) ambayo ilizinduliwa rasmi
Desemba, 2016, ambapo
hadi sasa tumewapa stadi za biashara endelevu wanawake 258 kutoka mikoa
6, ambayo ni Dar es Salaam, Arusha, Moshi, Mwanza, Morogoro na Zanzibar, na
tunaendelea kuwapatia ushauri wa kibiashara.”
“2JIAJIRI” inalenga kuondoa vikwazo
vinavyowakwamisha wanawake kama vile haki ya kumiliki mali,
kuanzisha ajira na sheria na kanuni ambazo zimewakwamisha wanawake
dhidi ya manufaa, biashara endelevu na maisha yaliyoboreshwa. Mradi huo
unatekelezwa kwa ushirikiano na Kituo cha Ushindani na Ujasiriamali Tanzania
(TECC) ambapo inawezesha wanawake wanaoshiriki kujitegemea, kuwa huru
kiuchumi na kudhibiti ustawi wao kiuchumi na kijamii,” Mukule alifafanua.
“Mradi huu upo katika mkondo wa
sera yetu ya benki ya uwekezaji kijamii ambayo inatoa kipaumbele
kujihusisha kijamii kuliko endelevu lengo lake kuu likiwa ni kunyanyua
maisha ya jamii,” alisema Mukule
Mukule alibainisha kuwa Benki
ya KCB kimsingi inatambua mchango mkubwa wa wanawake wanaoutoa katika sekta
binafsi hususani katika Ujasiriamali mdogo na wa kati (SMEs) na kuongeza
kuwa shughuli zao zinakumbana na changamoto nyingi pamoja na
upatikanaji wa mtaji, ufahamu finyu wa mambo ya kifedha, Utunzaji wa kumbukumbu
za kifedha, Kufikiwa na huduma za kifedha, Sera ongozi za biashara na
upatikanaji wa masoko
Mukule aliongeza, “Hivyo Lengo
letu kwa ujumla ni kuwezesha wafanya biashara wanawake wa Kitanzania kuandaa
mikakati ambayo inaboresha stadi zao na uwezo hivyo kuunda fursa nyingi za
kibiashara kwa ajili yao.”
Wale wanaofanikiwa kuhitimu
Programu ya KCB 2JIAJIRI wanapata fursa ya kipekee ya kujiunga na Klabu ya
Biashara ya KCB ambayo inawaunganisha na jumuia za
kibishara za kitaifa na kimataifa. Kadhalika wananufaika kwa kupata huduma ya
washauri watatu katika nyanja za Kifedha Kisheria na Masoko kwa kuwapatia
ushauri wa kibishara na kitaalamu.
No comments:
Post a Comment