Friday, May 12, 2017

KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU KUFUFUA MJADALA WA KATIBA MPYA

Kituo cha sharia na haki za binadamu nchini LHRC leo tarehe 12 mwezi mei kimekutanisha wawakilishi wa vyombo vya habari ikiwa ni waandishi pamoja na wahariri. Lengo likiwa ni kuhamasisha uhuishaji wa katiba mpya. 

Semina hiyo iliyofanyika hotel ya Seashells Millenium tower  jijini Dar es salaam iliongozwa na muadhiri wa chuo kikuu Prof. Khoti Kamanga akitoa mchanganuo  kuhusiana na mchakato wa katiba ulivyoanza na mpaka ulipokwama.

Prof. Khoti Kamanga akitoa ufafanuzi juu ya katiba ya mwaka 1977

Akitoa mawasilisho katika semina hiyo Prof Kamanga alipongeza jitihada za Rais wa awamu ya nne DK Jakaya Kikwete kwa kuweza kugundua kuwa katiba yetu ina mapungufu hivyo tunahitaji katiba mpya.

 Hivyo basi  mwaka 2011 aliweza kuunda baraza makini kwa ajili ya  kuanza kwa  mchakato wa katiba mpya.  Japo kuwa katiba iliyopatikana kutokana na maoni ya wananchi haikuweza kupewa nafasi lakini Rais alionyesha moyo wa kuitaka katiba mpya ambayo ni dira ya watanzania.

Waandishi wa habari pamoja na wahairi wa vyombo mbalimbali wakifuatilia mjadala
Prof Kamanga alisema kuwa sote tunafahamu kuwa katiba iliyopendekezwa haina tofauti sana katiba ya mwaka 1977 kwa kuwa zote zina mapungufu. Na miongoni mwa mapungufu hayo ni kumpa Raisi madaraka makubwa, na pia kuna kifungu kinachosema katiba ikijadiliwa bungeni ikashindikana kufikia muafaka basi inabidi itumike katiba ile ile yenye mapungufu. Lakini pia kingine ni kero za muungano ambazo bado hazina muafaka.

Waandishi wakiwa bize na kazi
Katiba ni chombo kinachotumika kwa watu wote hivyo basi inabidi ikubalike na pande zote sio kundi dogo la watu ndio likubali na wengine wapinge inakuwa sio katiba ya kufuata haki.

Katika semina hiyo yameweza kutolewa mapendekezo mbalimbali ikiwemo kuwa na ukomo wa wabunge wasiweze kuongoza zaidi ya awamu mbili. Lakini pia baadhi ya mambo yasiamuliwe bungeni mpaka wabunge waje kuomba Ridhaa kwa wananchi juu ya jambo husika.

Mbunge anapokosea au wananchi wameona mbunge wao hafai waende kuomba ridhaa kwa spika avuliwe nafasi yake. Lakini lingine mbunge asipewe nafasi ya uwaziri mbunge awe kama mbunge na waziri awe waziri ili asiweze kupewa feva kwenye baadhi ya mambo yake.

Waandishi wa habari wakiendelea kufuatilia mjadala
Katiba iweze kuboreshwa iwe ndogo kiasi kwamba hata kwenye mfuko wa suruali iweze kuingia isiwe mzigo mkubwa mpaka mtu aone uvivu kubeba. Na baadhi ya vifungu vitolewe vijadiliwe bungeni vibaki kama sheria ili kupunguza mlolongo mrefu wa vifungu.

Waandishi wa habari na wahariri wametakiwa kutangaza, kuchapisha machapisho na kutengeneza vipindi vinavyo hamasisha udaiji wa katiba mpya. Pia wameshauriwa kutochoka japo kuwa ni kazi ngumu na kutoogopa kudai katiba mpya kwani ndio msingi wa haki zote.

Waliweza kumshauri Raisi wa awamu ya tano DK. John pombe magufuli kuweza kurejesha tena mchakato wa katiba mpya kwani ndio kiu ya watanzania kwa sasa.

Prof.Khoti Kamanga akiendelea kutoa hoja




No comments: