Mtandao wa Jinsia nchini Tanzania TGNP leo Umeendesha warsha fupi iliyowakutanisha wanahabari na wanaharakati
mbalimbali kujadili bajeti ya wizara ya maji na umwagiliaji ya mwaka
2017/18.
Akiongoza warsha hiyo Mr. Melkizedek Karol alisema kuwa bajeti ya mwaka 2016/17 na
2017/18 kumekuwa na utofauti mkubwa sana kwa maana mwaka huu bajeti imeshuka
kwa zaidi ya bilioni 200. Kwa mwaka jana bajeti ilikuwa ni bilioni 915.1 kwenye mradi
wa maendeleo na kwa mwaka huu ni bilioni
623.6. na ikiwa imepanga 75% kwa pato la ndani na 25% pato la nje.
Na mwaka 2017/18 ikiwa miradi ya maendeleo 66% kwa kipato cha
ndani na 34%kwa kipato cha nje kwenye mipango ya maendeleo ikiwa imepangwa
kutumika 623.6 na wananchi wakiwa wanasubiri kuona kama kweli kiwango hicho
kitatolewa na serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Melkizedek Karol akifafanua jambo kwenye semina iliyofanyika ofisi za TGNP mtandao mabibo Dar es salaam |
Kwani mwaka uliopita wa fedha kulikuwa na mradi wa maji
kutoka ziwa victoria kwenda shinyanga kahama na tabora uliotengewa bilioni 22.4
na badala yake kutolewa milioni 500tu.
Lakini pia serikali imeweza kuainisha mambo mambo mengine ya
kufanyika kwenye bajeti yake ya maendeleo ya mwaka 2017/18 kama vipaumbele kwenye bajeti yake ya
bilioni 623.6 na mambo hayo kama yafuatayo.
Ukamilishaji wa miradi 509 katika halimashauri mbalimbali na
kuanza miradi mipya vijijini.
Kutekeleza miradi ya maji vijijini katika maeneo yenye ukame
na shida kama Dodoma ,singida pamoja na
shinyanga (kishapu DC)
Kuendesha upanuzi wa miradi ya maji vijijini vijiji 100
kandokando ya bomba kuu la KASHWASA.
Kuendelea na ujenzi
na ukarabati wa mabwawa
kukamilisha miradi inayoendelea na kuanza miradi mipya katika
kuboresha huduma ya maji katika jiji la dar es salaam.
Kuanza ujenzi wa miradi ya maji kutoka ziwa victoria kwenda
maeneo mbalimbali ikiwa pamoja na mji wa mwadui na kishapu.
Miradi ya maji mikoa na wilaya mpya.
Muwezeshaji akiwa anatoa elimu kwa walioudhuria semina |
Miongoni mwa
changamoto zinazoikabili sekta ya maji na umwagiliaji ni upungufu wa wataalamu
wa katika idra hiyo kwa kuwa
uhitaji ni mkubwa kuzidi waliopo. Kwa kuwa wanahitajika wataalamu 10,287 na
waliopo ni 2,290 kuna tofauti ya wataalamu 7,997 katika sekta hiyo.
Uwekezaji mdogo katika sekta ya maji na umwagiliaji kwa kuwa Tanzania ina hekta milioni 29.4 zinazofaa
kwa kilimo cha umwagiliaji na hadi sasa eneo linalomwagiliwa ni hekta 461,324
sawa na asilimia 1.6 ya eneo lote linalichangia chakula cha nchi nzima kwa
asilimia 24.
Kuweka vipaumbele vingi na hatimaye kushindwa kuvitimiza kwa
asilimia kubwa hii ikia ni kuweka vitu vichache kama vipaumbele ili kuweza
kuvitimiza kwa urahisi. Na siyo kuweka kila kitu ni kipaumbele mwisho miradi
kuishia kati bila kumalizika kwa kisingizio cha bajeti kutotosha.
Kuhujumu kwa miundo mbinu ya maji na madeni makubwa kwa
taasisi na idara za selikali.
Msafiri Shabani akichangia mada kwenye semina ya bajeti ya wizara ya maji na umwagiliaji |
Kulingana na hayo yote MR Melikizedek ameishauri selikali kupunguza vipaumbele na kuhainisha mambo machache kama
vipaumbele ili kuweza kuyatimiza kwa urahisi.
Selikali kuweka bajeti halisi na kiwango stahiki
ambacho inaweza kukipata na kupeleka kwenye wizara husika na siyo inaweka bajeti kubwa na kushindwa
kuitekeleza kwa asilimia kubwa kama ilivyoweka mwaka jana na ikaweza kutimiza
kwa asilimia 19 tu.
Mkurugenzi mtendaji wa TGNP mtandao Lilian Liundi akichangia hoja |
Wawezeshaji wakiorodhesha mapenekezo na matarajio ya wanaharakati |
No comments:
Post a Comment