Wednesday, May 24, 2017

WAKAZI WA DAR ES SALAAM WAFAIDI PIZZA YA BURE KUTOKA UBER




Dar es Salaam, Tanzania – Jumatano, tarehe 24 Mei, 2017….Uber leo watawakirimu abiria wake jijini Dar es Salaam kwa ‘pizza’ ya bure kama chakula cha mchana, hii ikiwa sehemu moja ya kampeni yetu ya kuongeza kuhitajiwa kwa kuwafurahisha wasafiri wanaoabiri Uber. Toleo hili maalum litakuwepo kwa muda wa saa 3 pekee (Saa 12:pm-3:pm) na litaweza kufikiwa na abiria wa Uber
katika maeneo ya kati ndani ya jiji.

Akizungumzia kuhusu shughuli hii, Meneja Mkuu wa Uber nchini Tanzania, Alfred Msemo alisema, “Sisi katika Uber, siku zote huwa tunatafuta njia bunifu, za kuhusisha na za usanifu zakuwachangamsha abiria pamoja na dereva-washirika wetu – bila shaka, wao ndio sababu ya yote tunayoyatekeleza. Kwa kugusa ya kitufe tu ifikapo muda wa chakula cha mchana hivi leo, abiria wa Uber watapokea kasha la pizza yenye ladha tamu, bila ya wao kuhitajika kuondoka ofisini mwao au makazi yao.”

Ili kupokea pizza ya bila malipo, wasafiri wa Dar es Salaam sharti wawe katika maeneo ya kati ndani ya jiji la Dar es Salaam. Ofa hii, itadumu kwa muda wa kati ya saa 12pm (saa sita mchana) hadi 03pm (saa tisa mchana) siku ya Jumatano, tarehe 24 Mei pekee, ni rahisi msafiri wa Uber anahitaji tukufungua programu ya Uber wakati huo wa kufunguliwa toleo, bonyeza bango la UberPIZZA chini ya skrini yako na kuomba UberPIZZA moja. Kama ombi limefanikiwa, dereva wa Uber atawasili mahali ulipo akiwa na UberPIZZA yako ya bure.

“Huku tukiwa tunapenda wengi wa abiria wetu iwezekanavyo wafaidike kutokana na kampeni hii, pizza za bure zitatolewa kwa misingi ya wanaokuja mwanzo- watawahi mwanzo. Ni wasafiri waliyo ndani ya eneo lililotajwa pekee watakaoweza kuona bango la UberPIZZA kwenye vifaa vyao;aliongeza Bw. Msemo

Kabla ya kampeni hii ya UberPIZZA, Uber walifanya kampeni ya kuzidisha mahitaji sawa na hii iliyopewa jina UberCHOMA ambapo wasafiri mjini Nairobi, Mombasa na Kampala walipokea nyama choma; ya bure kwa kubonyeza bango la UberCHOMA katika nyakati maalum. Meneja Mkuu wa Uber Afrika Mashariki, Loic Amado, alisema, “Tunajua kwamba moja ya mambo ambayo yanatufafanua sisi zaidi, hata katika miji mikuu, ni utamaduni wetu. Kampeni hii ya UberPIZZA jijini Dar es Salaam na ile ya awali ya UberCHOMA tuliyotekeleza katika miji ya Nairobi, Mombasa na Kampala ni moja tu ya njia ya kuadhimisha umaahiri wa utamaduni wa wana Afrika Mashariki na inatuunganisha na abiria wateja wetu na dereva-washirika wetu - kwa njia ambayo ni ya kukumbukwa.”

No comments: